0


 

WASHAMBULIAJI wa kimataifa wa Taifa Stars, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu, wanaocheza TP Mazembe, juzi Alhamisi usiku walifanya ziara ya kushitukiza kwenye hoteli ya La Rose walipoweka kambi wachezaji wa Azam.
Washambuliaji hao tegemeo wa Stars waliwasili hotelini hapo muda wa saa mbili usiku kwa hapa Lubumbashi (saa tatu usiku kwa Tanzania) na kuzungumza machache na wachezaji pamoja na viongozi wa timu hiyo.
Samatta aliukosa mchezo dhidi ya Azam Jumatano iliyopita kwani alikuwa hajarejea hapa Lubumbashi kutokea Urusi alikokwenda kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa kwenye klabu ya CSKA Moskow.
Mkurugenzi wa Azam, Jamal Bakhresa, alipata fursa ya kuzungumza machache na Samatta na kumshauri acheze tena msimu mmoja na Mazembe kabla ya kuondoka kabisa kwenda kutafuta maisha Ulaya huku pia akimtaka Ulimwengu kupambana zaidi.
“Kila mtu uwanjani alituambia kuwa tumepona kutokana na kukosekana kwa Samatta, wanasema ungetufunga hata mabao matatu peke yako, inaonekana wewe ni mchezaji muhimu sana hapa,” alisema Bakhresa.HABARI ZA SOKA NA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Post a Comment

 
Top