Kesi
ya Feisal Mohammed anayeshukiwa kuwa mlanguzi mkubwa wa Pembe za ndovu
Afrika Mashariki inatarajiwa kuendelea hii leo jijini Mombasa. Feisal
amekuwa rumande kwa majuma mawili sasa baada ya kunyimwa nafasi ya
kuachiliwa kwa dhamana.
Feisal Mohammed anatarajiwa kuanza
kujitetea mbele ya Mahakama ya Mombasa , dhidi ya mashtaka ya kumiliki
na kulangua kilo 314 ya pembe za ndovu zilizopatikana bandarini Kenya.
Ameshinda akila maharagwe tangu Desemba baada ya mahakama kukataa
kumwachilia kwa dhamana wiki mbili zilizopita, ikisema kuna uwezo
atahepa nchii hii Kesi yake ikiendelea. Mshukiwa alikamatwa nchini
Tanzania Desemba mwaka jana, miezi sita baada ya kesi yake kuanza, huku
upande wa mashtaka ukisema alitorokea huko baada ya kuarifiwa kuwa
anatafutwa na Polisi. Feisal Mohammed ametajwa na Polisi wa Kimataifa
Interpol kama mkuu wa kikundi sugu kinacholangua pembe za ndovu.KWA HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment