0
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesema mikoa yote ya Tanzania itakuwa imeunganishwa kwenye mfumo wa dijitali ifikapo Machi mwakani.
 Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Profesa John Nkoma, aliyasema hayo jana ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mkutano wa siku moja kuadhimisha Siku ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT) ya Jumuiya ya Mawasiliano Afrika (ATU).
 Alisema mikoa iliyokuwa imesalia ya Ruvuma, Mtwara, Iringa na Lindi licha ya baadhi ya wananchi wake kupata huduma za matangazo kupitia visimbuzi mbalimbali lakini bado haijaingizwa rasmi katika mfumo huo.
 Kukamilika kwa huduma hiyo katika mikoa hiyo kutafanya nchi nzima sasa kupata huduma za kidijitali ambayo inalenga kuwasaidia wananchi kupata matangazo bora.
Kuhusu mkutano huo unaotarajiwa kufanyika Desemba 4, mwaka huu, Profesa Nkoma alisema, lengo lake ni kuwakutanisha wadau kutoka ndani na nchi ya nje kubadilishana uzoefu wa namna ya kuboresha huduma za sekta hiyo.
“Zaidi ya washiriki 200, wanatarjiwa kushiriki mkutano huo. Mwingine umefanyika jana Desemba 5, mwaka huu uliohusisha watangazaji wa televisheni.”

Post a Comment

 
Top