Akiwasilisha maazimio hayo mwenyekiti wa PAC Mhe. Zitto Kabwe
amesema bunge pia linapendekeza serikali kuangalia uwezekano wa kuinunua
mitambo ya IPTL na kuikabidhi kwa Tanesco,pamoja kamati za kudumu za
bunge zichukue hatua za haraka kabla ya mkutano wa 18 wa kuwavua nyazifa
zao wenyeviti wa kamati za bunge waliotajwa kuhusika na kashfa
mabilioni ya fedha katika za Escrow.
Kwa upande wake kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni ni Mhe.
Freeman Mbowe amewata viongozi kutambua kuwa wanamamlaka ya kulinda
rasilimali za nchi na kumtaka waziri mkuu kuwa mkali zaidi kwa kuchukua
hatua na asisubiri mpaka bunge lifikie katika hatua ya mivutano,huku
makamu mwenyekiti wa kamati ya PAC Mhe. Deo filikunjombe amepongeza
bunge kukubali kamati hiyo.
Waziri wa nchi ofisi ya Rais mahusiano na utaribu Mhe.Stephen
Wassira amesema jambo lolote linaloweza kuvunja umoja na kurudisha nyuma
maendeleo haliwezi kuwa sera ya CCM ambapo amepongeza makubaliano
yaliyofikiwa kati ya CCM na vyama vya upinzani.
Akihitisha mkutano wa 16 na 17, waziri mkuu mheshimiwa mizengo
pinda amewahakikishia wabunge na wananchi kwa ujumla kuwa serikali
itaendelea kusimamia rasilimali za nchi kwa faida ya watanzania wote, na
kuahidi wale wote watakao patikana na jinai za kuvunja sheria za nchi
watachukuliwa hatua.Ambapo ameahirisha bunge hadi tarehe 27 januari
mwakani.ITV
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.