0

???????????????????????????????Waandishi wa Habari kutoka mkoani Katavi wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi baada ya kumalizika kwa mkutano kati ya Tume na Waandishi hao.

Na Kibada Kibada-Mpanda Katavi.
Imeelezwa kuwa Watanzania hawaoni thamani ya kupiga kura kwa sababu hata siku moja hawajawahi kunyimwa nafasi ya kuchagua viongozi wanaowataka kwa kutumia haki yao ya kidemokrasia.
Akifungua Mkutano wa siku  moja wa waandishi Habari na Tume ya Taifa ya Uchaguzi  unaohusu uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya kwanza na matumizi ya Teknolojia mpya ya Biometric Voter Registration uliofanyika Mjini Mpanda Mkoani Katavi,  Mjumbe wa Tume ya Taifa ya  uchaguzi  Prof.Amon  Chaligha amesema  watanzania walio wengi hawaoni thamani ya kupiga kura, hivyo vyombo vya Habari vinao wajibu Mkubwa wa kuelimisha umma juu ya  umuhimu wa kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura.
Zoezi  la uboreshaji daftari la wapiga kura unatarajia kufanyika mwezi septemba mwaka huu kwa maandalizi ya uchaguzi Mkuu wa Madiwani ,wabunge na Rais wa Jamhuri wa Tanzania  mwezi oktoba mwaka 2015.
Akifafanua zaidi alisema   Mataifa mengine  ambayo raia wake walinyimwa uhuru wa kupiga kura, wao wanaona thamani kubwa sana ya  kupiga kura, na ndio maana wanajitokeza kwa wingi katika kupiga kura kwenye chaguzi zao.
Akizungumzia  maandalizi ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa kutumia Teknolojia ya Biometrik Voter Registration amesema hii ni awamu ya kwanza ya mfumo huo wa BVR, hivyo watu wajitokeze kujiandikisha  kwa kutumia mfumo huo mpya.
Awali Kamishina wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Gregory Kaijage amesema Tume inatarajia kuboresha Daftari la kudumu la wapiga kura kwa awamu.
Amesema  demokrasia  inasema kila mtu ana haki ya kupiga kura kuchagua na kuchaguliwa katika nafasi za uongozi unaokuwa ukifanyika kwa kufuata utaratibu kwa mujibu wa sheria za nchi..
Akiwasilisha mada inayohusu maandalizi ya uboreshaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura  kwa kutumia teknolojia ya Biometric Vote Registration (BVR) ameeleza kuwa Tume inatarajia kuboresha Daftari la kudumu la wapiga kura awamu ya kwanza hivi karibuni na maandalizi yake tayari yamekamilika kwa sehemu kubwa.
Akifafanua zaidi amesema kuwa Tume ya Taifa ya Uchanguzi imepewa jukumu la kisheria kuandikisha wapiga kura  na kuboresha  Daftari la  hilo kwa ajili ya uchaguzi Mkuu wa Rais wa  Jamhuri wa Tanzania.
 Akizungumzia matumizi ya biometric katika zoezi la uandikishaji , amesema Tanzania  haitakuwa nchi ya kwanza kuingia katika mfumo huu wa BVR kwani tayari  umekwishatumika katika nchi mbalimbali zikiwemo za kiafrika ingawa alieleza mafanikio hayo yaliambatana na changamaoto mabalimbali za kiteknolojia na kimfumo.
Alizitaja baadhi ya nchi za kiafrika zilizokwisha tumia mfumo huo kuwa ni pamoja na Nigeria 2007,Ghana 2009,Liberia2005,Guinea 2005,Mali2005,Uganda 2008,Kenya 20013,Zambia2008Afrika Kusini na Zanzibar 2009 na Tanzania itatumia mfumo huu katika uandikishaji wa wapiga kura tu.

Post a Comment

 
Top