Waandishi
wa Habari kutoka mkoani Katavi wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe
wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi baada ya kumalizika kwa mkutano kati ya
Tume na Waandishi hao.
Na Kibada Kibada-Mpanda Katavi.
Imeelezwa
kuwa Watanzania hawaoni thamani ya kupiga kura kwa sababu hata siku
moja hawajawahi kunyimwa nafasi ya kuchagua viongozi wanaowataka kwa
kutumia haki yao ya kidemokrasia.
Akifungua
Mkutano wa siku moja wa waandishi Habari na Tume ya Taifa ya
Uchaguzi unaohusu uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura awamu
ya kwanza na matumizi ya Teknolojia mpya ya Biometric Voter Registration
uliofanyika Mjini Mpanda Mkoani Katavi, Mjumbe wa Tume ya Taifa
ya uchaguzi Prof.Amon Chaligha amesema watanzania walio wengi
hawaoni thamani ya kupiga kura, hivyo vyombo vya Habari vinao wajibu
Mkubwa wa kuelimisha umma juu ya umuhimu wa kujiandikisha katika
daftari la kudumu la wapiga kura.
Zoezi
la uboreshaji daftari la wapiga kura unatarajia kufanyika mwezi
septemba mwaka huu kwa maandalizi ya uchaguzi Mkuu wa Madiwani ,wabunge
na Rais wa Jamhuri wa Tanzania mwezi oktoba mwaka 2015.
Akifafanua
zaidi alisema Mataifa mengine ambayo raia wake walinyimwa uhuru wa
kupiga kura, wao wanaona thamani kubwa sana ya kupiga kura, na ndio
maana wanajitokeza kwa wingi katika kupiga kura kwenye chaguzi zao.
Akizungumzia maandalizi
ya uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa kutumia
Teknolojia ya Biometrik Voter Registration amesema hii ni awamu ya
kwanza ya mfumo huo wa BVR, hivyo watu wajitokeze kujiandikisha kwa
kutumia mfumo huo mpya.
Awali
Kamishina wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Gregory Kaijage amesema Tume
inatarajia kuboresha Daftari la kudumu la wapiga kura kwa awamu.
Amesema demokrasia inasema
kila mtu ana haki ya kupiga kura kuchagua na kuchaguliwa katika nafasi
za uongozi unaokuwa ukifanyika kwa kufuata utaratibu kwa mujibu wa
sheria za nchi..
Akiwasilisha
mada inayohusu maandalizi ya uboreshaji wa Daftari la kudumu la wapiga
kura kwa kutumia teknolojia ya Biometric Vote Registration (BVR)
ameeleza kuwa Tume inatarajia kuboresha Daftari la kudumu la wapiga kura
awamu ya kwanza hivi karibuni na maandalizi yake tayari yamekamilika
kwa sehemu kubwa.
Akifafanua
zaidi amesema kuwa Tume ya Taifa ya Uchanguzi imepewa jukumu la
kisheria kuandikisha wapiga kura na kuboresha Daftari la hilo kwa
ajili ya uchaguzi Mkuu wa Rais wa Jamhuri wa Tanzania.
Akizungumzia
matumizi ya biometric katika zoezi la uandikishaji , amesema Tanzania
haitakuwa nchi ya kwanza kuingia katika mfumo huu wa BVR kwani tayari
umekwishatumika katika nchi mbalimbali zikiwemo za kiafrika ingawa
alieleza mafanikio hayo yaliambatana na changamaoto mabalimbali za
kiteknolojia na kimfumo.
Alizitaja
baadhi ya nchi za kiafrika zilizokwisha tumia mfumo huo kuwa ni pamoja
na Nigeria 2007,Ghana 2009,Liberia2005,Guinea 2005,Mali2005,Uganda
2008,Kenya 20013,Zambia2008Afrika Kusini na Zanzibar 2009 na Tanzania
itatumia mfumo huu katika uandikishaji wa wapiga kura tu.
Post a Comment