Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionHuenda ndege zikatengezwa bila madirisha katika siku za usoni.
Kampuni ya ndege ya Emirates imezindua ndege ambayo imetengezwa na madirisha bandia
Badala ya abiria kuweza kuona nje moja kwa moja, sasa watalazimika kutazama picha kutoka nje wakiwa ndani kwa kutumia kamera za fibre-optic
Emirates inasema kuwa hatua hiyo inatoa fursa ya kuondoa madirisha yote katika ndege za siku zijazo, swala litakalozifanya kuwa nyepesi na kuongeza kasi yake.
Rais wa Emirates Sir Tim Clark amesema kuwa picha hizo ni nzuri sana ikilinganishwa na picha zinazotazamwa kwa macho.
Madirisha hayo bandia yanapatikana katika chumba cha kwanza cha ndege aina ya Boeing 777-300Er .
Sir Tim aliambia BBC lengo lao ni kuwa na ndege isiyo na madirisha kabisa.
''Fikiria ndege isio na madirisha kabisa lakini unapoingia ndani kuna madirisha'', alisema.
Image captionMadirisha katika ndege ya kampuni ya Emirates
Wasiwasi wa kiusalama
Wafanyikazi wa ndege wanatakiwa kuona nje ya ndege iwapo kuna dharura, mtaalam wa usalama wa angani Profesa Graham Braithwaite wa chuo kikuu cha Cranfield University alisema.
"Kuweza kuona nje ya ndege katika dharura ni muhimu, hususan wakati ambapo dharura ya uokoaji inafaa kutekelezwa'', alisema.
"Wahudumu wa ndege watalazimika kuona nje katika dharura , kwa mfano wakati wa moto, kabla ya kufungua mlango na kuanza uokoaji- na kitu chochote ambacho kitahitaji nguvu kufanya hivyo haitakuwa rahisi kuidhinishwa na afisa wa usalama wa angani''.
Hatahivyo maafisa wa usalama wa angani kutoka mamlak ya kudhitibi anga barani Ulaya European Aviation Safety Agency alisema: Hatuoni changamoto yoyote ambayo haiwezi kukabiliwa ili kuhakikisha kuwa kiwango cha usalama sawasawa na kile cha ndege ambayo ina madirisha ya wahudumu wa ndege.
Profesa Braithwaite alisema kwamba kizuizi kikuu katika ndege isiyo na madirisha itakuwa abiria wanavyohisi kuhusu teknolojia hiyo.
'Hakuna mbadala'
Mtaalam wa maswala ya usafiri wa anga John Strickland alisema kuwa ndege zisizo na madirisha zitakuwa na sauti ya chini. hatua hiyo pia itapunguza matumizi ya mafuta iwapo ndege hiyo itakuwa nyepesi.
"Chochote kitakachopunguza uzani wa ndege kitapunguza utumizi wa mafuta'', alisema.
Hatahivyo, yeye binafsi alipendelea kutaka kuona nje ya ndege : Napenda kuwa na madirisha , kwangu mie madirisha bandia ''sio mbadala''.
Kupitia safu yetu ya mahusiano, leo nimekuletea makala maalum hasa kwa wanawake kutokana na malalamiko ya wanawake wengi kuwapoteza waume zao. Ki...Read more »
kuzoeana baina ya wanandoa ni jambo zuri, kwa maana ya kila mmoja kumfahamu mwenzake, lakini kuzoeana huku kunaweza kuzalisha dharau hususani kwa...Read more »
Image captionMaandamano yamefanyika mjini Nairobi siku ya Jumatatu kulalamika kuhusu tuhuma za ubakaji katika shule ya Moi Girls Nairobi
Walimu pamoj...Read more »
Operesheni ya mwisho ya Tundu Lissu imefanyika na kumalizika salama.
Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), alifanyiwa op...Read more »
Haki miliki ya pichaAFPImage captionBado muswada unahitaji kupitishwa na Rais wa Rwanda Paul Kagame kabla ya kuanza kufanya kazi.
Bunge nchini Rwanda...Read more »
Post a Comment
aprieztmkrdezign
218168578325095
Emoticon
Click to see the code! To insert emoticon you must added at least one space before the code.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.