Chelsea imemsajili mshambuliji wa Arsenal Olivier Giroud kwa mkataba wa miezi 18 utakaogharimu £18m.
Mchezaji huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 31, anaondoka arsenal baada ya kufunga maba 105 katika mechi 253 tangu asajiliwe kutoka klabu ya Ufaransa ya Montpellier kwa kitita cha £12m mnamo mwezi Juni 2012.
Borussia Dortmundpia wamethibitisha kumsajili mshambuliaji wa Chelsea Michy Batshuayi hadi mwisho wa msimu huu.
- Arsenal kileleni baada kuitikisa Sunderland.
- Arsenal yashinda na kupanda juu ya Manchester United
- Arsenal kuchuana na Liverpool EPL
Awali Dortmund ilimuuza Pierre-Emerick Aubameyang kwa Arsenal.
Wakati huohuo Manchester City wamejiondoa katika makubaliano ya kumsajili winga wa Leicester Riyad Mahrez wakidai kwamba uhamisho wake ungeigharimu klabu hiyo dau kubwa la £95m.
Siku ya Jumanne mchezaji huyo alikuwa amewasilisha ombi la kuondoka katika klabu yake ya Leicester
Post a Comment