0
Ryan SessegnonHaki miliki ya pichaREX FEATURES
Image captionRyan Sessegnon
Kuna uwezekano mkubwa kwamba Liverpool watamruhusu Philippe Coutinho, 25, kuhamia Barcelona mwezi huu wa Januari kwa £140m. (Times)
Chelsea wanamtaka meneja wa Atletico Madrid Diego Simeone achukue nafasi ya Antonio Conte katika klabu hiyo mwisho wa msimu. (Times )
Chelsea wamezidisha juhudi zao za kutaka kumnunua kiungo wa kati wa Everton na England Ross Barkley, 24, na pia wameulizia kuhusu uwezekano wa kumnunua mshambuliaji wa England na West Ham Andy Carroll, 28. (Mail)
Mchezaji wa Celtic na Scotland Kieran Tierney, 20, amejumuishwa katika orodha ya mabeki wa kushoto ambao Manchester United wanawatafuta kuimarisha safu yao ya ulinzi, pamoja na kinda wa Fulham Ryan Sessegnon, 17. (Daily Record)
Paris St Germain wanatarajiwa kutoa ushindani kwa Tottenham katika kutafuta saini ya Sessegnon ambaye thamani yake imekadiriwa kuwa £30m. (Mirror)
Juventus wana imani kwamba watafanikiwa kumchukua Emre Can kutoka Liverpool bila kulipa ada yoyote mwisho wa msimu.
philippe coutinhoHaki miliki ya pichaREUTERS
Klabu hiyo ya Serie A imemuahidi mchezaji huyo wa miaka 23 mshahara wa £85,000 kwa wiki. (Guardian)
Manchester United wameanzisha mazungumzo ya kuongeza mikataba ya wachezaji wane kwa mwaka mmoja. Wachezaji hao ni viungo wa kati wa Uhispania Juan Mata, 29, na Ander Herrera, 28, beki wa England Ashley Young, 32, na beki Mholanzi Daley Blind, 27. (Mirror)
Manchester United wanataka sana kumnunua beki wa kushoto wa Juventus Sandro lakini wanavunjwa moyo na Juve kutotaka kumuuza mchezaji huyo wa miaka 26. (Express)
Tottenham wanatarajiwa kutoa mikataba mipya yenye donge nono zaidi kwa mshambuliaji wa England Harry Kane, 24, na beki wa Ubelgiji Toby Alderweireld, 28. (Independent)
Marseille wanamnyatia kiungo wa kati wa Arsenal Jack Wilshere lakini mchezaji huyo wa miaka 26 anataka kusalia na Gunners. (Mail)
Jack WilshereHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionJack Wilshere
Mkufunzi mkuu wa Monaco Leonardo Jardim amesema hana nia ya kumuuza mshambuliaji wake Mfaransa Thomas Lemar, 22, kwa Liverpool mwezi huu. (Liverpool Echo)
Meneja wa Paris St-Germain Unai Emery amefungua mlango kwa winga wa Brazil Lucas Moura, 25, na mwenzake wa Ufaransa Hatem Ben Arfa, 30, kuihama klabu hiyo Januari. (L'Equipe)
Mbelgiji Thibaut Courtois, 25, anakaribia kutia saini mkataba mpya Chelsea baada ya klabu hiyo kumpa ujira wa zaidi ya £200,000 kwa wiki, hatua itakayomfanya kuwa kipa anayelipwa pesa nyingi zaidi duniani. (Telegraph)
Beki wa Chelsea David Luiz, 30, anataka sana kuondoka klabu hiyo na anatumaini Real Madrid watamtaka. (Mundo Deportivo - kupitia Express)
Mkufunzi mkuu wa Newcastle Rafa Benitez anatafakari uwezekano wa kutaka kumnunua nahodha wa Watford Troy Deeney, 29. (Northern Echo)
Sandro RamirezHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionSandro Ramirez
Newcastle na Burnley nao wanataka kumnunua kiungo wa kati Mhispania Jonathan Viera, 28, kutoka Las Palmas. (Telegraph)
Sunderland wanakaribia kumchukua mshambuliaji mchanga wa Liverpool Ben Woodburn mwenye miaka 18 kwa mkopo. (Star)
Everton wanataka kumnunua kiungo wa kati wa Nice na Ivory Coast Jean Michael Seri, 26. (Sky Sports)
Meneja wa Everton Sam Allardyce hataki kumwachilia mshambuliaji Sandro Ramirez, 22, atoke nje kwa mkono Januari lakini anasema hana usemi wowote kuhusu hilo. (Liverpool Echo)
Crystal Palace wamewasilisha ofay a kutaka kumnunua beki wa kati wa Lille Ibrahim Amadou, 24. (Sun)
Besiktas wanataka kumnunua mshambuliaji wa Leicester na Algeria Islam Slimani, 29. (Leicester Mercury)
Islam Slimani alipokuwa Sporting LisbonHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionIslam Slimani alipokuwa Sporting Lisbon
Barcelona nao wanakaribia kumchukua beki wa kati wa Palmeiras ambaye ni raia wa Colombia Yerry Mina, 23. (Marca)
Manchester City nao wamesalia makini sana kutafuta walinzi sokoni kutokana na mahitaji ya kuwa katika michuano mingi. (Manchester Evening News)
Tamko la Bayern Munich kuhusu kiungo wa kati wa Schalke Leon Goretzka limekera klabu hiyo, na kuimarisha nafasi ya Liverpool kumnunua mchezaji huyo wa miaka 22. (Star)
Meneja wa zamani wa Bundesliga Jos Luhukay ni miongoni mwa wanaopigiwa upatu kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Carlos Carvalhal klabu ya Sheffield Wednesday. (Yorkshire Post)

Post a Comment

 
Top