Image captionCyril Ramaphosa amechaguliwa kuwa kiongozi mpya wa chama tawala cha ANC nchini A-Kusini .
Cyril Ramaphosa amechaguliwa kuwa kiongozi mpya wa chama tawala cha ANC nchini A-Kusini .
Ramposa ambaye alikuwa makamu wa rais wa chama hicho aliweza kumshinda mpinzani wake Nkosazana Dlamini-Zuma, ambaye ni waziri wa zamani na alikuwa mke wa rais Zuma kwa kura 2440 kwa 2161.
Kwa sasa Ramaphosa ameoneka kuwepo kwenye nafasi kubwa ya kuwa rais katika uchaguzi wa mwaka 2019.
Hata hivyo Cyril Ramposa amekuwa kiongozi wakati ambao Afrika kusini inakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zinafanya mambo hayendi sawa katika taifa hilo lenye uchumi mkubwa barani Afrika .
Cyril Ramaphosa ni mtu wa aina gani?
Cyril Ramposa alizaliwa tarehe 17 mwezi novemba mwaka 1952 mjini Soweto, ndio mwanasiasa tajiri zaidi Afrika Kusini ,utajiri wake unakisiwa kuwa ni dola milioni 450.Tangu ujana wake Ramposa alikuwa na ndoto ya kuwa mwanasiasa shupavu na hiyo ndio ilimfanya kujiunga na uongozi wa chama cha wafanyakazi .
Image captionRamposa akiwa na Nelson Mandela
Na wakati chama cha ANC kilipochukua uongozi wa Afrika kusini mwaka 1994,alitamani sana kuwa naibu wa mwasisi wa Afrika Kusini mpya ,Nelson Mandela lakini pale Mandela alipompuuza na badala yake kumteua Jacob Zuma inasemekana kuwa bwana Ramaphosa alisusia hata sherehe za kuapishwa kwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini vilevile alisusia kuchukua wadhifa wowote wa uongozi katika serikali mpya ya Afrika Kusini .
Badala yake bwana Cyril Ramaphosa ambaye alisomea uwakili alihiari kuwa mbunge na mwenyekiti wa bunge la katiba ambalo lilishughulikia kutengeneza katiba ambayo ilisifiwa sana duniani.
Haki miliki ya pichaAFPImage captionRais Jacob Zuma na Naibu wake Ramaphosa
Badaye Ramaphosa alishangaza wengi alipojiuzulu kutoka kwenye siasa na kushughulika zaidi katika biashara zake,lakini mwaka 2012 alishawishika tena na kurudi kwenye siasa na kuwa na ilipofika mwaka 2014,alipanda zaidi na kuwa makamu wa rais Zuma.
Na wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema kurudi kwake Ramaphosa kwenye chama cha ANC kulirudisha imani ya wananchi wengi licha ya kuwa chama hicho kilikuwa kinakabiliwa na kashfa nyingi za kisiasa.
Msanii mkongwe wa BongoFleva nchini Afande sele atangaza rasmi kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) mwezi huu march mbele ya Rais Dkt. Maguf...Read more »
Mfanyabiashara maarufu kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Moise Katumbi ambaye sasa amejitosa kwenye ulingo wa siasa, anazindua chama chake a...Read more »
Image captionNkurunzinza amekuwa rais wa Burundi tokea mwaka 2005
Chama tawala nchini Burundi CNDD/FDD kimemtangaza Rais Pierre Nkurunzinza kama kion...Read more »
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeibuka kidedea katika uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Siha mkoani Kilimanjaro baada ya Tume ya Uchaguzi (Nec), ...Read more »
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionTrump ana handaki ndani ya nyumba yake ya Mar-a-Lago estate - lakini halina uhusiano wowote na yeye kuwa...Read more »
Kupitia safu yetu ya mahusiano, leo nimekuletea makala maalum hasa kwa wanawake kutokana na malalamiko ya wanawake wengi kuwapoteza waume zao. Ki...Read more »
kuzoeana baina ya wanandoa ni jambo zuri, kwa maana ya kila mmoja kumfahamu mwenzake, lakini kuzoeana huku kunaweza kuzalisha dharau hususani kwa...Read more »
Post a Comment
aprieztmkrdezign
218168578325095
Emoticon
Click to see the code! To insert emoticon you must added at least one space before the code.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.