0

Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Rajab AbdulKahal maarufu Harmonize ametoa Msada wa Fimbo30 kwa Chama cha Wasioona Kilichopo Mkoa wa Mtwara Zenye Thaman ya Shilingi Million1 na Laki8 kama njia mojawapo ya kuwafariji walemavu wa macho katika kipindi hiki cha Sikukuu.

Katika Salam zake Hamornize amesema alipata taarifa ya kuwa chama Hicho kinauhitaji wa Fimbo kwa ajili ya Matumizi ya Kutembelea hivyo kuamua Kuleta Fimbo hizo ambapo Mahitaji ya Fimbo kwa kiasi kikubwa yanahitajika.

Aidha amewaomba baadhi ya Wadau wenye uwezo kujitokeza na kutoa Msaada ili kupunguza changamoto ambazo zinawakabili watu wenye ulemavu wa Macho.

Akizungumzia Kuhusiana na ziara yake Mkoani Mtwara Harmonize anasema bado Ataendelea Kutoa Msaada kulingana na anachopata na ataendelea kutembea asasi mbalimbali zenye mahitaji maalum ili kuweza Kusaidi.
Msanii wa Muziki wa kizazi Kipya Harmonize akimkabidhi Fimbo 30  katibu wa chama cha Wasioona Mkoani Mtwara Ally Ismail.

 Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Harmonize katika Picha ya Pamoja na chama cha watu Wasioona Mkoani Mtwara Mara baada ya kukabidhi Msaada wa Fimbo kwa walemavu wa Macho Mkoani Mtwara.
 Harmonize akimuongoza Kushuka Ngazi katibu wa Chama cha Wasioona Ally Ismail katika Makabidhiano ya Msaada wa Fimbo za kutembelea kwa watu wenye Ulemavu.


 Harmonize akiwa na Rafiki yake Sarah Akiongea na Wanachama wa Chama cha watu Wasioona kabla ya Kukabidhi Fimbo30 kwa ajili ya kutembelea.

Post a Comment

 
Top