0
Wakazi wa Sinai na Magugu, Babati, Manyara wakishiriki kwenye zoezi la usajili wa Vitambulisho vya Taifa.


Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imeanza zoezi la usajili wa watu katika wilaya zote za mikoa ya Manyara na Singida ambalo linalenga kuwapatia Vitambulisho vya Taifa. 

Kuwapatia Vitambulisho wananchi kutasaidia kutambulika pale wanapotaka kugawiwa pembejeo za Kilimo, kupata leseni za udereva na biashara, kusajili namba za Simu, kumiliki Ardhi, kupata mikopo, kufungua akaunti benki na matumizi mengineyo yanayohitaji utambulisho. 

Mratibu wa Usajili wa mikoa ya Manyara na Singida, Thomas William ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Biashara amesema watu wengi wanajitokeza kusajiliwa baada ya kuelimishwa kuhusu umuhimu wa Vitambulisho vya Taifa

Post a Comment

 
Top