0
Mesut Ozil
Image captionMesut Ozil
Kiungo wa kati wa Arsenal Mesut Ozil anaitaka Barcelona kumlipa dola 370,000 kwa wiki ili kujiunga nao mwezi Januari.Mkufunzi wa Gunners yuko tayari kumwachilia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 ili asijiunge na Man United wakati mkataba wake utakapokamilika mwishoni mwa msimu ujao. (AS)
Paris St-Germain imeanzisha mazungumzo na kiungo wa kati wa Manchester United Marouane Fellaini. Kandarasi ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 inakamilika mwishowe wa msimu huu. (Le10Sport - in French)
Julian Draxler
Image captionJulian Draxler
Liverpool imewasiliana na PSG kuhusu uhamisho wa mkopo wa kiungo wa kati wa Ujerumani Julian Draxler, 24. (L'Equipe via Daily Mail)
Mkufunzi wa zamani wa West Ham Slaven Bilic amekataa mwaliko kutoka kwa West Brom kuzungumzia kuhusu wadhfa ulio wazi wa mkufunzi wa klabu hiyo. (Daily Mail)
Stoke, West Ham, Everton na Southampton wana hamu ya kumsajili mshambuliaji wa Watford Odion Ighalo. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 alielekea katika klabu ya ligi ya Superleague nchini China Changchun Yatai mwezi Januari. (Tutto Udinese, via Stoke Sentinel)
Juan Mata
Image captionJuan Mata
Kiungo wa kati wa Uhispania Juan Mata, 29, anataka kuongeza kandarasi yake katika klabu ya Manchester United na amesema kuwa anaweza kucheza hadi kufika miaka 40.. (ESPN)
Mshambuliaji wa Ubelgiji Eden Hazard, 26, amesema kuwa atasalia hadi mwisho wa msimu kutathmini hatma yake katika klabu ya Chelsea (Canal+ via Independent)
Mkufunzi wa Watford Marco Silva
Image captionMkufunzi wa Watford Marco Silva
Watford wana imani kwamba mkufunzi Marco Silva hataki kujiunga na Everton kwa kuwa anatafuta nyumba katia eneo la Hertfordshire. (Daily Mirror)
Everton inaonekana kuvunjika moyo katika kujaribu kuwashawishi The Horhets kuwaruhusu kujadiliana na Silva. (Hertfordshire Mercury)
Crystal Palace itashindana na West Ham katika kumsajili kiungo wa kati wa Bournemouth Harry Arter, 27, mnamo mwezi Januari. (Daily Mirror)
Beki wa Uingereza wa zamani Sol Campbel
Image captionBeki wa Uingereza wa zamani Sol Campbel
Beki wa Uingereza wa zamani Sol Campbel amesema kuwa ana hamu ya kuwa mkufunzi wa timu ya Marekani. (ESPN)
Beki wa Ufaransa Eliaquim Mangala, 26, amekiri kwamba huenda akaondoka Manchester City mnamo mwezi Januari.(Sun)
Winga wa Algeria Riyad Mahrez, 26, hajatoa ishara yoyote kwamba anataka kuondoka Leicester kulingana na mkufunzi Claude Puel. (Leicester Mercury)

Post a Comment

 
Top