0


 WAJUMBE wa  bodi ya  Mfuko  wa  Rais  wa  kujitegemea  uwezeshaji  kiuchumi  wakiongozwa  na  Mwenyekiti  wa  bodi NATU MSUYA wakitembelea vikundi  vya  wajasiriamali wilaya  Lindi 


kukosekana  kwa  umeme  wa  uhakika  mkoani  Lindi kumeelezwa kuwa  kunachangia Wajasiriamali   kushindwa  kufikia malengo  yao ya  uzalishaji  


Malalamiko  hayo  yametolewa  na  baadhi ya  wafanyabiashara  wakati  walipokuwa  wanatoa taarifa za za  vikundi  kwa bodi ya  mfuko  wa  Rais  wa  kujitegemea  walipokuwa  kwenye  ziara  ya  kutembelea  vikundi  vilivyokopeshwa  mikopo kupitia  mfuko  huo

 Akisoma  taarifa  hiyo   mwenyekiti  wa  kikundi  cha  HIJI  WORK SHOP, Hiji Twalibu timu  ya  alisema  tatizo  la  kukosekana kwa  huduma ya  wa  uhakika  unachangia kiwanda  kushindwa  kufikia  malengo  ya  uzalishaji   na  kusabisha  mapato  kuwa madogo

Twalibu alisema  kuwa  imekuwa  utamaduni  wa  kawaida  kuona umeme  haupatika siku  mzima baadhi ya maeneo  yakipata huduma hiyo kwa mashaka  na kiasi kidogo ikiambatana na mgawo na  kukatika katika kusiko weza kuelezwa.

Alisema  umekuwa  tatizo sababu baadhi wamekuwa wakipata huduma hiyo usiku wa manane na alfajiri umeme unakatwa jambo ambalo limesababisha malalamiko mengi ya wateja .

 Zakia Litonji alisema shirika la umeme mkoani humu limeshindwa kutoa huduma  kwa wakati na kusababisha usumbufu kwao na wakosesha mapato ambayo wanayatumia kulipa kodi kwenye mamlaka ya mapato Tanzania(TRA) 
   
Kwa upande Afisa  Habari  wa  Tenesco mkoa wa  Lindi Francis  Mbelwa  alikiri kuwepo kwa tatizo hilo na alisema hivi sasa huduma hiyo ya umeme inatolewa kwa mgawo kwa sababu uwezo wa ufuaji wa umeme umepungua kutokana na kuharibika kwa Generata   moja  iliyoko  mkoa  Mtwara  kwenye  kituo  cha  kufulia  umeme.

Mbelwa  alisema tatizo  litaondoka  baada  ya  kuletwa  genarate  mpya  mbili  zilizoombwa ili kuongea nguvu  ya  uzalishaji uvuaji  umeme  kwenye  kituo  cha  kugawa  umeme mikoa  ya  Lindi  na  Mtwara 

Awali Afisa  Mikopo  tawi  la  Lindi Zeitun  Halfan  alitoa  taarifa kwa  bodi  hiyo  kuwa  mfuko  tawi  la Lindi  umefanikiwa  kutoa  mikopo  144 yenye  thamani  ya  shs  milioni 73 kati  hiyo  mikopo 30 yenye  thamani  ya  shs milioni 13,100,000 imetolewa  kwa  vijana , na  mikopo 114 yenye  thamani  ya  shs milioni 69 900,000 zimetolewa  kwa  wanawake  na  mikopo  29  yenye  thamani  ya  shs  milioni 10,800,000 kwa  vikundi nne  vya  wajasilimali  wanawake wilaya  Ruangwa.

Zeitun alisema  vikundi  87 vyenye  wajasilimari 165, vijana 35 na wanawake 130 zilivyoko wilaya   Lindi  na Ruangwa vinajishughulisha katika shughuli mbalimbali ikiwemo ufugaji,utengenezaji wa sabuni na vikapu,na  wilaya Lindi, vinajihusisha, kilimo, bustani,ufugaji  wa kuku,  mashamba  ya  chumvi, ushonaji, na  uselemara.

 WAJUMBE wa  bodi ya  Mfuko  wa  Rais  wa  kujitegemea  uwezeshaji  kiuchumi  wakitembelea vikundi  vya  wajasiriamali  TOP FIVE  Mkwaya  wilaya  Lindi
 WAJUMBE wa  bodi ya  Mfuko  wa  Rais  wa  kujitegemea  uwezeshaji  kiuchumi  wakitembelea vikundi  vya  wajasiriamali  HIJI wilaya  Lindi
 WAJUMBE wa  bodi ya  Mfuko  wa  Rais  wa  kujitegemea  uwezeshaji  kiuchumi wakionozwa  na  mwenyekiti NATU  MSUYA   wakitembelea vikundi  vya  wajasiriamali wilaya  Lindi
WAJUMBE wa  bodi ya  Mfuko  wa  Rais  wa  kujitegemea  uwezeshaji  kiuchumi   wakiongozwa  na  mwenyekiti NATU MSUYA wakitembelea vikundi  vya  wajasiriamali wilaya  Lindi

Post a Comment

 
Top