0


Mkuu  wa  mkoa  wa  Lindi Godfray  Zambi   amewaomba  Radhi    wakulima  wa  korosho  mkoani  Lindi  kwa  kitendo  cha  kukosa  pembejeo ya Kilimo  Sulphur  kwa  wakati  baada  ya  serikali  kuahidi  kutoa  pembejeo  hizo  bure

Zambi alichukua   hatua   hiyo  baada  ya  Meneja  wa  Ubanguaji  korosho kutoka  bodi ya Korosho  (CBT) Eng  Shabani  Yahaya  kueleza  kuwa wakulima  wa korosho  mkoani  Lindi  wasitegemee  dawa  zinazotolewa  na  bodi  ya  koshoro  kwani  hazitaweza  kutosheleza , hivyo kuwataka  wakulima  ho kununua  pembejeo hizo  Madukani.

 Zambi  alisema kitendo cha  bodi ya  korosho  kutangaza  kusambaza  dawa  bure  kimewafanya  wakulima  kuacha   kununua  pembejeo   hizo, hali  ambayo  imesababisha  mikorosho  mingi  kutopuliziwa  hadi  sasa.

Alisema serikali imekuwa  ikitukanwa na  wakulima Kila  kona  kutokana  na utendaji mbovu  wa  usambaza pembejeo kwa  wakulima.

 wadau  wa kilimo , Ufuta, Korosho , na Mihogo   mkoani Lindi   walikuwa  kwenye  kikao  na  Bank  ya  wakulima TADB wakitoa Fursa  zinazotolewa na  bank  hiyo. Chanzo:Sauti ya kusini blog

Post a Comment

 
Top