0
Kijana mmoja ambaye jina lake halijafahamika mara moja amenusurika kufa kutokana na kichapo kutoka kwa wananchi wenye hasira baada ya kutapeli pesa shilingi 370,000/= katika kibanda cha duka la Mpesa katika soko la Kambarage kata ya Kambarage Mjini Shinyanga.
Tukio hilo limetokea leo Julai 6,2017 majira ya saa nane mchana ambapo kijana huyo alifika kwenye kibanda cha Mpesa cha Robert Masesa kilichopo jirani na soko la Kambarage na kutapeli kiasi hicho cha pesa.

Akisimulia kuhusu mkasa huo mmiliki wa kibanda hicho, Masesa alisema majira ya saa tano kijana huyo alifika kibandani hapo akitaka huduma ya kutoa pesa ,lakini alipoombwa simu yake iangaliwe ujumbe mfupi wa maneno katika simu kama udhibitisho akawa hana simu.

Alisema alipombana akasema ametumia namba ya mwingine ndipo akaagizwa amfuate ,lakini kabla hajaondoka akaja mteja mwingine kutoa pesa ndipo akanuti yake ikasema namba yake imefungiwa.

Masesa alieleza kuwa baada ya kupata ujumbe huo ,ndipo akashtuka kuwa ametapeliwa na alipomuita kijana huyo alianza kutimua mbio na baiskeli ndipo akapiga yowe na hatimaye kijana kunaswa na na wananchi kisha kuanza kupewa kichapo.

Hata hivyo wakati wananchi hao wakitembeza kichapo ndipo wakafika askari polisi na kumnusuru kutoka katika kichapo hicho ambacho kiliambatana na mawe makubwa na kuokoa uhai wake na kisha kuondoka naye kwenda kituo cha polisi.

Post a Comment

 
Top