Afrika wiki hii kwa picha : 12 - 18 Mei 2017 0 Kimataifa 10:51:00 A+ A- Print Email Baadhi ya picha bora kutoka barani Afrika na zile za Waafrika wakiwa sehemu mbali mbali duniani. Haki miliki ya pichaEPAImage captionMchuuzi akiwauzia wapita njia na wenye magari panya waliochomwa eneo la Salima, Malawi, siku ya Jumatatu. Panya waliochomwa wanapendwa sana na watu nchini Malawi na biashara yake hunoga sana hasa vijijini.Haki miliki ya pichaEPAImage captionSiku hiyo hiyo kobe huyu wa aina ya 'ploughshare' aliokolewa nchini Malaysia baada ya kusafirishwa kinyemela kutoka Madagascar. Maafisa walipata kobe 330. Kobe hao walikuwa wamewekwa kwenye masanduku amabayo yalidhaniwa kusafirisha mawe kutoka uwanja wa ndege wa Antananarivo, nchini Madagascar.Haki miliki ya pichaAFPImage captionSiku ja Jumamosi, wanahabari waliruhusiwa kupiga picha za miili ya watu waliofariki zama za kale iliyohifadhiwa huko Misri. Waakiolojia waliipata miili 17 isiyo ya watu wa familia ya kifalme katika jangwa. Kando ya maiti hizo, kulikuwa na makala ya dhahabu iliyochapishwa zamani sana.Haki miliki ya pichaAFPImage captionSiku hiyo hiyo mwendeshaji pikipiki wa mashindano ya pikipiki wa Afrika Kusini aliwatumbuiza watu waliofika kwenye sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya kuwepo kwa jimbo la Lagos, nchini Nigeria.Haki miliki ya pichaAFPImage captionUjenzi unaendelea katika kambi ya wakimbizi wa kutoka Sudan kusini katika eneo la al-Algaya, nchini Sudan, siku ya Jumatano.Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionSiku ya Jumatatu, mwanamke huyu alikuwa ameketi karibu na mahakama ya kikatiba mjini Johannesburg, Afrika Kusini, ambako kulikuwa na maandamano ya kumtaka Rais Jacob Zuma aondoke mamlakani.Haki miliki ya pichaAFPImage captionWakulima wajitayarisha kuuza mifugo wao kwenye maonyesho katika soko kubwa zaidi la kilimo barani Afrika huko Bothaville, Afrika Kusini siku ya Jumanne.Haki miliki ya pichaAFPImage captionAskari kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo anatazama michoro ya grafiti kwenye kuta za ikulu ya zamani ya rais, siku ya Jumatatu...Haki miliki ya pichaJOHN WESSELSImage captionIkulu hiyo ya zamani iliyokuwa makao ya Rais wa zamani wa DRC Mobutu Sese Seko inapatikana Nselel, kilomita 40 nje ya mji mkuu Kinshasa.Haki miliki ya pichaAFPImage captionSese Seko alifukuzwa na vikosi vya waasi wakiongozwa na Laurent-Desire Kabila mwaka wa 1997 baada ya miaka 32 ya utawala. Alikufa miezi mitatu baadaye, huko Morocco. Picha ni kwa hisani ya AFP, EPA, Getty Images na Reuters
Post a Comment