0


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein  amewataka  mabalozi wanaokwenda kuiwakilisha Tanzania nchi za nje  kuhamasisha  wawekezaji kuja kuwekuza hapa nchini hasa katika sekta ya viwanda.
                 


Akizungumza na Mabalozi Wateule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, waliofika Ikulu kumuaga pamoja na kufanya nae mazungumzo, Rais Shein amesisitiza kuwa sekta ya viwanda imepewa kipaumbele na kutiliwa mkazo mkubwa na Serikali zote mbili.
Mabalozi hao ni pamoja na Balozi Emmanuel Nchimbi ambaye anakwenda kuiwakilisha Tanzania nchini Brazil, Balozi Mbelwa Kairuki anaekwenda nchini China, Balozi Geogre Kahema Madafa anaekwenda Italy, Balozi Profesa Elizabeth Kiondo anakwenda nchini Turkey.

Wengine ni Balozi Dk. James Msekela UN nchini Geneva, Balozi Samwel Shelukindo anaekwenda Paris, France na Balozi mteule Lt. Jeneral (Mstaafu) Paul Mella anaekwenda D.R. Congo.
Dkt. Shein ameeleza haja ya Mabalozi hao kuitangaza Zanzibar na Tanzania nzima kiutalii ambapo kwa upande wa Zanzibar sekta hiyo imekuwa ni muhimu kutokana na kuchangia asilimia 80 ya pato la Taifa.

Ambapo amesisitiza haja ya kuvitangaza vivutio vya kitalii vilivyopo nchini vikiwemo Mbuga za wanyama, sehemu za kihistoria, fukwe na vyenginevyo.

Nao Mabalozi hao walimthibitishia  Dk. Shein kuwa wamepokea maelekezo yote aliyowapa na kuahidi kuyafanyia kazi hasa kwa maeneo maaluma ya Zanzibar na Tanzania Bara.

Post a Comment

 
Top