0


Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli, amemteua Rogers Sianga kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini.
                        


Kamishna Mkuu Sianga atasaidiwa na Mihayo Msikhela ambaye anakuwa Kamishna wa Operesheni na Fredrick Kibuta ambaye anakuwa Kamishna wa Intelijensia.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amemteua Dkt. Anna Peter Makakala kuwa Kamishna Mkuu wa Uhamiaji.

Kabla ya uteuzi huo Dkt. Makakala alikuwa Mkuu wa Chuo cha Uhamiaji Moshi, kilichopo Mkoani Kilimanjaro.

Uteuzi huu unaanza mara moja na wateule wote wataapishwa siku ya Jumapili Februari 12.

Post a Comment

 
Top