0


Jitihada za kurejesha miundombinu ya shule ya Msingi Mlengu kata ya Kigala wilayani Makete iliyoharibiwa na mvua iliyoambatana na upepo mkali Februari 16 mwaka huu bado zinaendelea

Akizungumza na mwandishi wetu kwa njia ya simu, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Yusto Mwinuka amesema mvua hiyo iliharibu vyumba vitatu vya madarasa ambavyo ni vya darasa la awali, la pili na la tano, ambapo wamelazimika kubomoa madarasa yote hayo na kuanza kuyajenga upya

Amesema licha ya changamoto hiyo kuwakumba lakini wanafunzi wote bado wanasoma baada ya kukarabati chumba kimoja cha darasa kilichokuwa hakitumiki ambapo sasa kinatumiwa na wanafunzi wa darasa la 5 na chumba kingine kinatumiwa kwa zamu na darasa la awali na la pili

Kwa upande wake diwani wa kata ya Kigala Mh Kevin Nguvila amewaomba wadau wenye moyo kuona namna ya kuunga mkono jitihada zinazofanywa na wananchi wa kijiji cha Mlengu kuhakikisha madarasa hayo yaliyoezuliwa mapaa yanajengwa upya ili wanafunzi waendelee na masomo yao kama awali

Amesema kwa hivi sasa tayari ameshakaa na wananchi wake kuhusu suala la kurekebisha miundombinu hiyo ambao wamekubaliana kuchanga, na tayari ujenzi wa madarasa hayo upya unaendelea
Sikiliza sauti za viongozi hao(Diwani na Mwalimu Mkuu)

Post a Comment

 
Top