0
Tokeo la picha la lindi


Mwaandishi wetu
IMEBAINIKA baadhi ya madereva wa Pikipiki au maarufu boda boda mkoani Lindi wamekuwa wanawaweka wanafunzi  shule za msingi na sekondary ujauzito wakati wakiwa bado shuleni mwaka jana.
Hayo yaliyobainishwa na mkuu wa mkoa wa Lindi Godfrey Zambi wakati alipokuwa akizungumza na wananchi, viongozi wa ngazi ya wilaya serikali ya kijiji pamoja na kata ya Litingi, wilayani humo, alisema kwamba moja ya wilaya kuna wanafunzi wa sekondary saba walipatiwa ujauzito na madereva hao, mwaka jana.
Tatizo linalowakuta wanafunzi hao kuomba lifti kwenda shuleni hapo ni moja ya chanzo cha kupatiwa ujauzito wanafunzi wanaosoma mbali na shule zao  kutoka nyumbani kwenda shuleni.
Aliongeza kwa kusema kwamba wazazi toeni nauli kuwapa wanafunzi siyo mnaawaacha wapewe lifti, ni hatari kwa vijana hao.
Aidha aliwataka viongozi wa serikali za vijiji hadi wilaya kuwachukulia hatua kali za kisheria wale wote wanawaweka wanafunzi mimba.
'Hivi karibuni kuna mzee mmoja alimweka mimba mwanafunzi sasa yuko ndani anatumikia kifungo.
'Mimi nasema nataka hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi yao siyo kuwaachia wazazi na wati mimba kudanganyana'' alisema Zambi.
Alisema kwamba kaaeni macho na umakini hasa hawa wanafunzi wa kike hizi lifti wanazozitaka ni changamoto ni lazima wazazi mjitoe kuwasaidia wakiwa bado mashuleni.
Aidha aliwashari wazazi kutoa michango ya shuleni hasa kwenye ujezni wa vyoo ili kusaidia wanafunzi pamoja na walimu kukaa maeneo yenye usalama kiafya

Post a Comment

 
Top