0
Tokeo la picha la choo cha kisasa


 Mwandishi wetu
Watu 1,200 mjini Lindi mkoani humo wanatarajiwa kufikishwa Mahakama ya mwanzo kutokana kutuhumiwa kutojenga vyoo katika majumbani mwao wanakoishi,
Hayo yaliyobainishwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Joumary Satura leo wakati alipokuwa akiwasilisha taarifa yake mbele ya ya wajumbe wa baraza la madiwani kwenye kikao cha baraza la madiwani cha nusu ya mwaka 2016/2017 mjini hapa.
Alisema kwamba mamlaka iliamuwa kuchukuwa hatua hiyo baada ya kujiridhisha kaya hizo wanaishi bila ya kuwa na vyoo na kusababisha hatarishi kutokea magonjwa ya milupuko ya kuhara na matumbo.
Satura alisema kwamba elimu zinapitishwa mara kwa mara juu ya umuhimu wa kuwa na vyoo, lakini jamii nayo inakuwa na wakati mgumu kutekeleza elimu hiyo.
'Tumeamuwa kuchukuwa hatua hiyo ili kuweza kukomesha kwa wananchi wengine ambao hawana na vyoo kuweza kujenga'alisema mkurugenzi huyo.
Aliongeza kwa kusema kwamba jamii inapaswa kutiaa sheria zinazowekwa na mamlaka husika na kuzitekeleza kwa wakati unaotakiwa.
Aidha alisema kwamba barua za kuitwa zilishaanza kutolewa juu ya watuhumiwa hao kwenda mahakamani.
Alisema kwamba ufuatiliaji unandelea ili kuweza kubaini kaya nyingine ambazo hazina vyoo.
Hivi karibuni Serikali ya mkoaa wa Lindi ilishwai kusema kwamba wilaya za Kilwa na Liwale zinaongoza kwa wananchi wake kutkuwa na vyoo mkoani humo.
Mkuu wa mkoa wa Lindi Godfrey Zambi aliyasema hayo katilka kijiji cha Tingi wilayani Kilwa.
Alisema kwamba kwa hiyo wananchi wajenge vyoo na ikiwezeka mpaka mashuleni kama hakuna huduma hiyo wachangie

Post a Comment

 
Top