Ripoti
zinasema Bw Kerry Johnson yuko hatarini kutumikia kifungo cha kati ya
miaka mitano na 18 gerezani kutokana na mashtaka yanayomkabili.
Ilisemekana alikuwa akicheza Kamari katika kasino ya kifahari ya Mardi Gras lakini akaishiwa na pesa.
Aliondoka
na kufululiza hadi katika benki ambapo alimtishia mhudumu kwamba
alikuwa na bomu na atalipua benki hiyo kama hatapewa anachotaka.
Kulingana
na mashirika ya habari, alifanikiwa kuiba dola 5,000 (Sh515,000) lakini
badala ya kutorokea mahali ambapo hangepatikana, alirudi katika kasino
kuendelea kucheza Kamari.
Polisi
walimkamata siku iliyofuata na upekuzi ulifanywa nyumbani kwake
uliwawezesha kupata karatasi iliyofanana na ile aliyoandikia vitisho
alivyompa mhudumu wa benki, pamoja na kofia iliyofanana na ile
iliyonaswa kwenye video ya CCTV wakati wa wizi.
Inasemekana kulikuwa pia na kitita kikubwa cha pesa zilizofichwa kochini mwake.
Mashirika
ya habari yalisema alipofikishwa mahakamani, Bw Johnson alidai alikuwa
ametumia dawa siku hiyo na hakuwa anajifahamu, lakini alikiri jamaa
aliyeonekana akiiba kwenye video ni yeye.

Post a Comment