0

        Mkuu wa wilaya ya Liwale,mhe. Sarah Chiwamba
Viongozi  wa  chama  cha  ushirika  Mahonga  wilaya  Liwale  mkoani Lindi  Imani  Mtesa  katibu  mkuu  Isa  Mpunja  katibu  msaidizi  ,  Saidi  Linda  mwenyekiti  wa  chama  na  Modester  Makota  Makamu  mwenyekiti  wa  chama  hicho  wanashikiliwa  na jeshi  la polisi  baada ya  agizo la  mkuu  wa wilaya  Sarah  Chiwamba  kutaka  washikiliwe  kwa  kosa la  kutowalipa  wakulima  wa  korosho  zaidi ya  100  wakati  minada yote  imelipwa  katika  chama  hicho.

Hatua  hiyo  imekuja  baada ya  wakulima  wa  korosho  wa  chama hicho  kuandamana  hadi  ofisi  ya  mkuu  wa wilaya  hiyo , kuulalamikia  oungozi  wa  chama  hicho  kutowalipa  fedha   zao  za korosho  msimu 2017/18

Post a Comment

 
Top