Simba SC
imeendeleza wimbi la ushindi katika michuano
ya Mapinduzi inayoondelea
visiwani Zanzibar baada ya hapo jana
kushinda kwa ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Timu ya KVZ ya Zanzibar
Shukrani za
dhati zimuendee mfungaji wa goli hilo Jamali Simba Mnyate bao ambalo
limepatikana katika dakika ya 44 ya kipindi cha kwanza
Bao hilo limepatikana baada ya mabeki wa kati wa KVZ
kutega mtego wa kuotea ambapo Simba walifanikiwa kutegua mtego huo na Jamal Simba Mnyate akafanikiwa kufunga bao
lake la kwanza katika michuano hiyo
tangu kuanza kwake mwaka huu.
Kabla ya hapo kulikuwa na mchezo wa awali
uliopigwa majira ya saa 10:30 za
jioni ikiwakutanisha Jang’ombe Boys dhidi ya URA
na Jang’ombe Boys ikafanikiwa
kushinda mabao 2-1
Ushindi huo walioupata timu ya Jang’ombe dhidi URA ni ushindi wa kwanza kwa vilabu vya
Zanzibar kupata ushindi kwa vilabu kutoka nje ya Zanzibar vinavyoshiriki ligi
ya mapinduzi yaliyozinduliwa rasmi tar 30 january 2016
Matokeo hayo yanaifanya Simba kufikisha point 6
huku wakiwa wamecheza michezo 2 na kulazimika kukaa
kileleni mwa kundi A huku mabigwa watetezi
URA wakiwa nafasi ya pili wakiwa
wamecheza michezo miwili na kunyakua point 6
Post a Comment