Dar es Salaam
Young African (wakimataifa) wamedhiirisha umahiri wa kilitandaza soka katika michuano ya mapinduzi baada ya jioni
ya leo kupata usindi wa pili mfululizo kwa kufanikiwa kuifunga Zimamoto bao
2 bila ya majibu mchezo ambao umepigwa majira ya saa 10:30 za jioni katika uwanja wa Amani
Shukurani ziende kwa
mfungaji ya mabao hayo Saimon msuva
aliyefunga mabao hayo katika kipindi cha kwanza na kuifanya yanga
ikienda mapumziko ikiwa inaongoza mabao 2-0 ambapo hadi dakika 90 zinamalizika
hakukuwa na mabadiliko yeyote.
Ushindi huo unaifanya Yanga kufikisha point 6 na magoli
nane na kulazimika kuketi katika nafasi ya kwanza kwa msimamo wa kundi
B,huku nafasi ya pili ikisalia kwa Azam wakiwa wamecheza mchezo mmoja na
kufanikiwa kunyakua point 3 na goli 1
Dar es Salaam
Young African ilishuka dimbani kwa mara ya kwanza jumatatu ya tarehe 2-1-2017
na kufanikiwa kuwalaza kwa mabao 6-0 Jamhuri kutokea Kisiwani Pemba
Hata hivyo
mashindano hayo yataendelea majira ya saa 2:30 za usiku kwa
kuwakutanisha Mabingwa wa Africa Mashariki na kati dhidi ya Timu ya Jamhuri
kutokea kisiwani Pemba
Ikumbukwe Azam anaingia katika mchezo huo akiwa na
kumbukumbu nzuri ya kushinda goli 1-0 katika mchezo wake cwa kwanza dhidi ya Zimamoto
na Jamhuri nayo inashuka katika mchezo huo wakiwa na kumbukumbu mbaya ya
kupoteza mchezo wao wa awali dhidi ya yanga baada ya kufungwa bao 6-0
Post a Comment