NA
SELEMANI,ZANZIBAR
Mashabiki na wanachama wa Club ya Simba Visiwani Zanzibar wanamatumaini makubwa ya
kunyakua ubigwa wa kombe la mapinduzi kutokana na uimara unaooneshwa na wachezaji wa kikosi chao.
Simba ya Dar es Salaam inatarajia kushuka dimbani
kwa ajili ya kucheza mchezo wake wa kwanza dhidi ya Taifa Jang’ombe majira ya
saa mbili za usiku katiak Uwanja wa Amanani Visiwani Zanzibar
Timu ya Taifa ya Jang’ombe leo itashuka dimbani kwa mara ya pili kucheza
na Simba huku ikiwa na kumbukumbu nzuri ya kushinda kwa ujumla wa bao 1-0 katika
uchezo wao wa mwanzo dhidi ya watani wao wajadi Jang’ombe Boys mchezo ambao
umepigwa siku ya ufunguzi wa michuano hiyo
desembar 31 mwaka jana
Katika kuelekea mchezo huo mshabiki wa Simba aliejitambilisha kwa jina la Omari wa Tawi la Mlingotini Amani visiwani Unguja amesema
matumaini yao kushinda mchezo huo wa leo na mechi nyenginezo na hawana wasi
wasi na kikosi chao kwakua lengo lao ni kuchukua ubigwa wa kombe la Mapinduzi
“unajua Simba ni timu kubwa na wala huwezi
kuifananisha na Timu nyengine yoyote hapa Tanzania hivyo sisi kama wanasimba
kwa umoja wetu hapa Zanzibar tunamatuamini makubwa sana ya kunyakua ubingwa wa
Mapinduzi hata wa Ligi kuu bara” alisema Omari
Nae makame Awadhi ambae pia ni mshabiki wa Club ya
Simba Visiwani hapa amesema simba ni lazima ichukue ubigwa kutokana na uwezo
unaooneshwa na wachezaji wake katika ligi kuu bara huku akimtolea mfano Pastory Athanas mshambuliaji chipukizi wa Simba waliomsajili katika kipindi
cha dirisha dogo akitokea Stend United ya Mkoani Shinyanga
“ukweli ni kwamba Simba ndio timu bora zaidi hapa Tanzania,maana
hata ukiangalia mchezaji mmoja mmoja wana vipaji vya hali ya juu tofauti na
Yanga ambao wachezaji wao wengi wazee, embu angalia Yule kijana aliyetoka stend(Pastory
Athanas) kacheza michezo miwili tu lakini ni moto wa kuotea mbali, sasa kama hivyo
kweli hakuna kinachoizuiya Simba kuchukua ubigwa huu wa Mapinduzi wala ligi kuu Tanzania bara” alisema Awadhi.
Simba ni miongoni mwa vilabu vyenye rekodi nzuri ya michuano ya mapinduzi
kuanzia mwaka 2007 ambao wamelichukua mara tatu mwaka 2008,2011 na 2015
ukilinganisha na yanga ambao wamelichukua mara moja ambao ni mmwaka 2007 huku azam ikichukuwa mara mbili 2012 na 2013
Angalia hapo chini nimekuwekea ratibiba ya mabingwa
wa kombe la mapindizi linalofanyika kila mwaka Zanzibar
ORODHA YA MABINGWA KOMBE LA MAPINDUZI
Mwaka Bingwa Mshindi wa Pili
2007 Yanga SC Mtibwa Sugar
2008 Simba SC Mtibwa Sugar
2009 Miembeni KMKM
2010 Mtibwa Sugar Ocean View
2011 Simba SC Yanga SC
2012 Azam FC Simba SC
2013 Azam FC Tusker FC
2014 KCCA Simba SC
2015 Simba SC Mtibwa Sugar
2016 URA Mtibwa Sugar
Mwaka Bingwa Mshindi wa Pili
2007 Yanga SC Mtibwa Sugar
2008 Simba SC Mtibwa Sugar
2009 Miembeni KMKM
2010 Mtibwa Sugar Ocean View
2011 Simba SC Yanga SC
2012 Azam FC Simba SC
2013 Azam FC Tusker FC
2014 KCCA Simba SC
2015 Simba SC Mtibwa Sugar
2016 URA Mtibwa Sugar
Post a Comment