Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameagiza walimu wanaoishi mbali na
shule hali yakuwa shule zao zina majengo wahame mara moja na kuishi karibu na
maeneo yao ya kazi
Amesema haifai kuacha
walimu waishi mbali na maeneo ya shule kwani hali hiyo inachangia uchelewaji
kazini na inapunguza muda wa kuwasimamia wanafunzi au kuwasaidia jioni pale
wanapohitajika kufanya hivyo.
Ametoa agizo hilo wakati akizungumza na
wakazi wa kijiji cha Chingumbwa, kata ya Mbekenyera, wilayani Ruangwa kwenye
mkutano uliofanyika kwenye uwanja wa shule ya msingi kijijini hapo.
Pia Waziri Mkuu amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya
ya Ruangwa, Andrea Chezue asimamie zoezi hilo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha
anapunguza walimu walioko Ruangwa mjini na kuwahamishia shule za vijijini
ambako kuna upungufu wa walimu.
Post a Comment