Waumini
wa dini ya Kikristo nchini wametakiwa kusheherekea sikukuu ya Krismas kwa
kufanya Ibada pamoja na mambo yanayompendeza Mungu.
Akizungumza
na Liwale blog Mchungaji Charles Kiyengo kutoka Kanisa la RGC Welezo amesema
watu wengi wamepoteza dhana ya sikukuu ya Krisimas ambayo ni kuwahimiza waumini
kufanya ibada badala yake wamekuwa wakifanya mambo kumchukiza Mungu.
Mchungaji
Kiyengo amesema waumini wa dini ya Kikristo wanapaswa kurudi katika dhana kuu ya sikukuu ya
Krismasi ambayo huwahimiza waumini wake kufanya ibada,kuwajali wagonjwa na watu wenye maisha magumu.
Nae
Mchungaji Gaudance Mihungo kutoka Kanisa la Deper Life Miembeni Unguja
amesema waumini wanatakiwa kusheherekea
sikukuu ya Krismasi kwa kuungana na
familia zao huku wakitafakari maana halisi ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo.
Nae
Mchungaji Philipo Kiyanda kutoka Kanisa la RGC Hanyegwamchana amesema kuzaliwa
kwa Yesu Kristo ni tukio
lililotabiriwa miaka mingi na halikuja
kwa kubahatisha bali ni kuwatoa watu katika maisha yasiyo na utakaso.
Amesema Krismasi haipo
kumsukuma mtu kufanya uovu bali ipo kwa ajili ya kumkumbusha mtu kufanya mambo
mema na kupokea baraka kwa kuwa Krismasi ni ukombozi wa mwanadamu kutoka kwa
Mungu.
Waumini wa dini ya
Kikristo nchini leo wanaungana na waumini wenzao duniani kuadhimisha kuzaliwa
kwa bwana na mwokozi wao Yesu Kristo takribani miaka 2000 iliyopita na Ujumbe
wa krismas wa mwaka huu ni haki na amani kwa wanyonge.

Post a Comment