0


Naibu Katibu Mkuu CCM Zanzibar  mh: Vuai Ali  Vuai leo amekabidhi gari  aina ya Kenta kwa Jimbo la Chumbuni  ili kutatua changamoto mbali mbali zinazowakabili jimboni  hapo.
 Naibu katibu mkuu zanzibar Vuai Ali  Vuai

 




Akikabidhi gari hiyo jimboni hapo ambayo imetolewa na  mbunge, mwakilishi na diwani wa  jimbo hilo mh: Vuai amesema gari hiyo itatumika  jimboni hapo   bila ya kujali itakadi ya chama chochote.
Kwa upande wao mbunge wa jimbo hilo mh: ussi salum pondeza na mwakilishi wake mh:miraji mussa khamisi wamewataka wananchi wa jimbo hilo kuondoa tofauti zao za kisiasa kwa lengo la kupeleka mbele maendeleo ya jimboni humo.


Mh mbunge wa jimbo la chumbuni   Ussi Salum Pondeza (kulia)
  
Akisoma Risala katika hafla fupi ya kukabidhi vifaa hivyo, Abrahman Abass alisema vifaa hivyo vimetolewa na viongozi wa jimbo hilo ambao ni Mbunge, Mwakilishi na Madiwani.

Alivitaja vifaa vyengine vilivyotolewa kuwa ni pamoja na Dawa za binadamu kwa ajili ya vituo vya Afya vya jimbo hilo pamoja na jezi za mpira wa miguu kwa timu za jimbo zenye usajili wa ZFA.

ZAIDI ya shilingi milioni 43 zimetumika kununua vifaa mbali mbali  vya Jimbo la Chumbuni Zanzibar, ikiwa ni utekelezaji wa ahadi zilizotolewa na Viongozi wa jimbo hilo kwa wananchi  katika Kampeni za Uchaguzi uliopita.

Post a Comment

 
Top