0


KATIBU wa Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya Taifa Zanzibar wa Idara ya Itikadi na Uenezi Mhe. Waride Bakari Jabu amewataka Wana CCM kuendelea kuthamini mchango wa hali na mali iliyotolewa na Waasisi wa Vyama vya ASP na TANU katika harakati ya kuwaletea Uhuru wananchi wa Tanzania Bara na Zanzibar.


Kauli hiyo ametoa katika nyakati tofauti alipokuwa akizungumza na Wanachama wa CCM wa Matawi wa Chaani, Mkwajuni, Nungwi na  Kijini ya Wilaya ya Kaskazini “A” ikiwa ni mfululizo wa ziara yake ya kukagua Uhai wa Chama Wilayani humo.

Amewataka Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla kuwa mstari wa mbele na kutumia mafanikio na changamoto za Waasisi hao, kama njia mojawapo ya kuendeleza mapambano ya kukumbuka na kuthamini kwa vitendo juhudi zao hizo.  


Amesema Waasisi wa vyama vya TANU na ASP walijitolea muhanga kuhakikisha Wananchi wa Tanganyika na Zanzibar wanakuwa huru   kutoka kwenye makucha ya wakoloni wa Kiingereza na Kisultani walozitawala  kwa mabavu nchi mbili hizo,  kwa zaidi ya miaka 150 iliyopita.

Bi. Waride amesisitiza haja kwa Wana CCM kuzidisha mashirikiano miongoni pamoja na kubuni mbinu na mikakati madhubuti ya kiuchumi itakayosaidia kwa kiasi kikubwa kukuza mapato ya Chama.

Ametoa wito kwa Viongozi na Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi pamoja na wananchi kwa ujumla wa Mkoa wa Kaskazini Unguja kudumusha suala zima la amani na utulivu uliodumu kwa miaka 53 sasa, kwa maslahi ya Taifa na wananchi wake.

Post a Comment

 
Top