Baada ya kupisha sherehe za Krismas hii leo, Ligi
kuu Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea kesho kwa kuchezwa mchezo mmoja katika
Uwanja wa Mabatini, Mlandizi Mkoani Pwani ambapo wenyeji Ruvu Shooting
watashuka dimbani kuwakaribisha washika bunduki za magereza Tanzania Prison
kutoka Jijini Mbeya
Huo utakuwa mchezo wa pili mfululizo kwa Ruvu Shootin
kucheza katika uwanja wake wa nyumbani katika mzunguko huu wa pili ulioanza
kutimua vumbi novembe 17,ambapo katika mchezo wa awali Ruvu wakiwa uwanjani
hapo walitoshana nguvu kwa kufungana bao moja kwa moja na Mtibwa Sugar Kutoka Wilayani
Turiani Mkoani Morogoro
Ruvu Shooting watashuka dimbani kesho kucheza mchezo
wao wa kumi na saba wa Ligi kuu Tanzania bara kwakua hadi sasa ipo katika nafasi
ya 9 katika msimamo wa ligi, wakiwa wamecheza michezo 16, wameachwa kwa nafasi mbili na wapinzani
wao Tanzania Prizoni kutokea juu, ambao wapo katika nafasi ya 7, michezo kumi na sita na point zao 22
Katika mchezo huo
Ruvu Shooting inahitaji kufanya vizuri ili ijiweke katika nafasi nzuri
ya kupigania kutoshuka daraja mwishoni mwa msimu.
Tanzania Prisoni wao wanashuka dimbani wakiwa wanakumbukumbu nzuri ya kushinda mchezo
wao wa kwanza uliochezwa Desember 18 dhidi ya Maji Maji ya Ruvuma mchezo ambao
ulipigwa katika uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya na Tanzania Prison ikafanikiwa kushinda
Goli mmoja kwa sifuri
Ligi hiyo itaendelea tena Mwaka 2017

Post a Comment