0
6WAKULIMA na wafugaji kutoka kata za Imalasongwe na Ubaruku katika halmashauri ya wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya wameilalamikia kampuni ya Highland Estate inayojishughulisha na kilimo cha mpunga wilayani humo kwa kitendo cha kuchepusha maji ya mto Balali hali ambayo inaathiri kwa kiasi kikubwa mtiririko wa maji katika mto Ruaha Mkuu na hivyo kuzorotesha shughuli za kilimo katika maeneo hayo.
Wakulima na wafugaji hao ktk maeneo hayo wamezungumza kuwa muwekezaji huyo amekuwa mara kwa mara akichepusha maji yam to Balali ambayo yanapashwa kutiririka ktk mto Ruaha Mkuu na hivyo kuathiri kwa sehemu kubwa maisha yao kwani wamekuwa wakikosa maji ya kwa ajili ya matumizi ya majumbani na ya kuendeshea kilimo na ufugaji.
Kwa upande wake Diwani wa kata ya Imalasongwe Bw Chuki Jeremiah anakiri kuwepo kwa tatizo hilo na kusema kutokana na kukosekana kwa maji wakulima na wafugaji hao wamekuwa wakivutana na muwekezaji huyo kwa muda sasa hali ambayo ktk siku za hivi karibuni imepelekea mauaji.
Afisa wa Maji wa Bodi ya Maji ya Bonde la Rufiji Bw Idrisa Msuya amesema amepokea malalamiko hayo na hivyo kumuagiza muwekezaji huyo kufuata utaratibu uliopo kinyume na hapo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Post a Comment

 
Top