0

Uongozi wa wachama cha wananchi (CUF ) mkoa wa Kusini Pemba umesema hawaitambui  ziara ya Profesa Ibrahimu Lipumba kisiwani Pemba ki chama kwani haiandaliwi na uongozi wa chama hicho mkoani humo na badala yake wamemtaka aende  kama Mtanzania.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa ulinzi na usalma wa chama hicho  mkoa wa Kusini Pemba Yusufu Salim Hussen ambae pia nimbunge wa jimbo la chambani  wakati alipokuwa akitowa taarifa kwa vyombo vya habari na viongozi wa majimbo na wa wilaya Chake na Mkoani.

 Wakizungumza kisiwani Pemba baadhi ya wanachama wachama CUF kisiwani Pemba wamesema Profesa Lipumba nimtanzania na hazuiwikuja Pemba kwa vile anahaki sawana mtanzania yeyote ila hawata kubali kuzungumzanae katika masuala ya chama.

Uongozi wa CUF mkoa Kusini Pemba wamefanya mkutano huo kufatia tetesi zilizo zagaa kisiwani Pemba kuwepo ziara ya Profesa Ibrahimu Lipumba hivi karibuni.

Chanzo:ITV

Post a Comment

 
Top