0


Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli ametoa msaada wa chakula na vinywaji kama zawadi ya sikuku ya Krismasi katika kituo cha wazee Bukumbi kilichop jijini Mwanza.

Akikabidhi zawadi hizo kwa niaba ya Rais Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela amewambia wazee hao kuwa pamoja na kusherekea sikukuu hiyo wasisahau kumuombea Rais kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuliongoza Taifa.


        Mkuu wa mkoa wa mwanza JOHN MONGELA

Mongela amesema serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali pamoja wizara husika wana mipango mizuri na wamejipanga ili kuboresha kituo hicho lengo likiwa ni kutatua kero na changamoto zinazowakabili  wazee ho.

Crement Bullo ni mzee anayeishi katika kituo hicho amesema wanaishukuru serikali kwa msaada wa chakula na kusema kuwa kwa sasa wana chakula cha kutosha lakini tatizo linalowafanya wanarudi mtaani kuombaomba ni kwa ajiri ya kupata hela ya kubadilisha mboga.

Naye afisa ugavi na manunuzi wa kituo hicho Jeremiah Nyanda amesema pamoja na kumshukuru Rais wanaiomba serikali kuwasaidia kutatua changamoto waliyonayo ya kukosa uzio pamoja na jiko ukizingatia kituo hicho kina walemavu wa ngozi hivyo kukosa uzio ni hatari kwa usalama wao.


Post a Comment

 
Top