0


Jeshi la polisi mkoa wa kusini unguja limejipanga kwa  kufanya doria yenye lengo la kunusuru na kudhibiti vitendo vya udhalishaji wa jinsia kwa watoto wanaokwenda kwenye maeneo ya kusherehekea sikukuu za chrimasi na mwaka mpya.

          Akizungumza na bahari fm huko tunguu mkoa wa kusini unguja RPC Kamandawa  Polisi  Juma  Sadi Khamis amesema kuwa kuelekea kipindi cha sikukuu ya krimasi na mwaka mpya pamoja na sherehe za mapinduzi ya Zanzibar amesema kuwa jeshi la polisi limejipanga kikamilifu kuwalinda watalii wanaofika kwenye sherehe hizo ili washerehekee sikukuu hizo kwa amani na utulivu.
Pia kamanda wa polisi mkoa wa kusini Unguja ametoa wito kwa wananchi kwa ujumla kusherehekea sikukuu ya krimasi na mwaka mpya kwa amani na utulivu.

Aidha amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi kwa kutoa taarifa mapema kwenye jeshi hilo iwapo watagundua kunataka ama kumefanyika vitendo vya uhalifu nchini.
          Aidha amewataka wamiliki wa nyumba za starehe walioruhusiwa wazingatie uhalali wa matumizi ya kumbi zao.

Post a Comment

 
Top