0


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam na kukagua eneo la ujenzi wa makazi ya askari wa Magereza unaotarajiwa kuanza baada ya wiki tatu zijazo. 
Waziri mkuu wa TANZANIA KASSIM MAJALIWA
 
Akizungumza na askari wa magereza kabla ya kufanya ukaguzi huo leo Waziri Mkuu amesema ziara yake hiyo, ni ufuatiliaji wa maagizo ya Mhe. Rais John Magufuli aliyoitoa wakati alipoenda kukagua gereza hilo Novemba 29 mwaka huu na kupokea taarifa ya uhaba wa nyumba za kuishi askari wa jeshi hilo takriban elfu 9 na 500 ambapo aliagiza kutafutwa kiasi cha sh. Bilioni 10 ili kupunguza tatizo hilo.


Waziri mkuu wa TANZANIA KASSIM MAJALIWA



Waziri Mkuu amesema amefarijika kukuta Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) wako eneo la kazi na wameanza kusafisha eneo hilo.
Amesema katika ziara alizozifanya kwenye mikoa mbalimbali, alitembelea magereza ya Isanga, Msalato mkoani Dodoma, Lindi, Singida na Keko jijini Dar es Salaam na kukuta nyumba za askari hazina viwango na kama zipo zimechakaa sana.
Awali, akitoa taarifa kuhusu ujenzi wa nyumba hizo, Kaimu Kamishna Jenerali wa Magereza, Juma Malewa amesema wanamshukuru Rais Magufuli kwa kuwapatia fedha za ujenzi wa makazi ya askari na kwamba jeshi hilo litafanya kazi zote zisizo za kitaalamu ili kuokoa fedha za Serikali na badala ya kulipwa watu binafsi, fedha hizo zitatumika kuongeza nyumba zaidi.

Post a Comment

 
Top