0


Ligi kuu tanzania bara imeendelea kurindima katika viwanja sita, katika Mikoa tofauti tofauti  hapa nchini,ambapo katika Uwanja wa Uhuru Jijini Dare es Salaam vinara wa ligi kuu  Simba wameendelea kujidhatiti kileleni baada ya kushinda bao moja kwa duara dhidi ya Jkt Ruvu katika mchezo ulioanza majira ya saa 10 jioni ya leo Jijini Dare es Saalam

 Goli hilo limepatikana katika dakika 45  lililofungwa na Muzamiru Yaasini baada ya shambulio kali lililofanywa na Simba katika dakika 44 na kusababisha wachezaji wa Jkt Ruvu kumzonga mwamuzi Hans Mabena wa Tanga aliyesaidiwa na Omar kambangwa wa Dar es Salaam na Khalfan Sika wa Pwani kwa madai kuwa kipa wao alikua amelala chini.

Katika kipindi cha pili Simba walionekana kutawala mpira zaidi na kupelekea kulisakama lango la wapinzani wao ambapo katika dakika Dk 49, Simba walimtoa Bukungu na nafasi yake ikachukuliwa na Hamad Juma ambapo jkt ruvu nao walifanya mabadiliko katika Dk 55, Ally Billa alitoka nje na kuingia  Najim Magulu
Dakika chache baadae Jkt Ruvu wakafanya mabadiliko kwa mara nyengine kwa kumuingiza   Atupele Green baadaya  Salim Gilla  kuumia

Licha ya mabadiliko hayo lakini bado Simba waliendelea kumiliki mchezo ambapo katika dakika 62 Mo Ibrahim alitoka na  nafasi yake ilichukuliwa na Jamal Simba Mnyate
Simba walienokana kutawala lango la Jkt zaidi lakini umakini waumaliziaji ulionekana kuwa mdogo zaidi katika kikosi hicho ambapo mwalimu Omog alilazimika kufanya mabadiliko mengine kwa kumtoa mkata umeme wao kutoka nchin Ghana Kotei  katika dakika 79 na kuingia Said Ndemla.
Karika mchezo huo Mshambuliaji Pastory Athanas aliyesajiliwa dirisha dogo mwezi huu kutoka Stand United akicheza kwa mara ya kwanza leo alionyesha kiwango cha hali ya juu na kuwafurahisha wanachama na mashabiki wa Simba.
Hii leo  akicheza kama mshambuliaji mbele ya lango la JKT, Pastory aliisumbua ngome ya timu hiyo ya Jeshi la Wananchi Tanzania na kukaribia kufunga mara kadhaa.
Kwasasa Simba inakaa kileleni ikiwa inajumla ya point 41,huku wakiwa wamecheza michezo 17 sawa na watani wao Yanga ambao wako katika nafasi ya pili na point zao 37 huku wakicheza michezo 17.
Kikosi cha Simba hii leo kilikuwa Kipa Mghana, Daniel Agyei alionyesha kiwango kizuri akiokoa michomo kadhaa ya hatari na kuizuia Simba SC kuruhusu bao, Jonas Mkude, Janvier Bukungu/Hamad Juma dk50, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Abdi Banda, Method Mwanjali, Shiza Kichuya, James Kotei/Said Ndemla dk79, Pastory Athanas na Mohamed Ibrahim/Jamal Mnyate dk62. 
Na Jkt Ruvu nao kiliundwa na: Hamis Seif, Salim Gilla, Michael Aidan, Frank Nchimbi, Yussuf Chuma, Kelvin Nashon, Edward Joseph, Hassan Dilunga, Hassan Materema, Mussa Juma/Kassim Kisengo dk80 na Ally Bilal/Atupele Green dk62.

Katika michezo mengine ya ligi kuu iliyochezwa leo, Maji Maji walishuka Dimbani wakiwa nyumbani Dhidi ya Azam na kufungana bao moja kwa moja,wakati Mbeya City walishuka katika Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya kuwakaribisha Toto Africa ya Mwanza  na kutoka suluhu ya bila kufungana
Huko Mkoan Mtwara Ndanda ya Mtwara 0-2 Mtibwa Sugar ya Morogoro, wakati Mwadui wameshinda goli 1-0 dhidi ya Mbao Fc ya Mwanza
Na huko kaitaba Kagera Sugar ameshinda goli 1-0 dhidi ya Stand United
Ligi hiyo kubwa zaidi kwa Tanzania bara itaendelea tena tarehe 26 kwa kupigwa mchezo mmoja katika Uwanja wa Mabatini kwa kuwakutanisha wenyej Ruvu Shooting v Tanzania Prisons [Mabatini, Mlandazi].


Post a Comment

 
Top