0

Ikiwa ni wiki chache zimepita baada ya Rais Rodrigo Dutetre wa Ufilipino kukiri hadharani kuwaua kwa kuwapiga risasi watu waliokuwa wanatumia dawa za kulevya nchini humo, nyingine iliyonifikia leo ni hli ya kuwatishia watumishi wote watakaobainika kujihusisha na rushwa kuwa atawarusha kutoka kwenye helikopta.
Rais Duterte amedai hii haitakuwa mara yake ya kwanza kufanya hivi kwahiyo watu wasidhani hamaanishi anachokiongea. Hili tamko lingine kutoka kwa raisi Dutetre wa Ufilipino kwa wala rushwa nchini kwake.
>>“If you are corrupt I will fetch you using a helicopter to Manila and I will throw you out. I have done this before, why would I not do it again?” -Dutetre
Akimaanisha ‘Kama wewe ni mtoaji au mpokeaji rushwa nitakamata kwa helikopta mpaka Manila na nitakutupa nje. Nimeshawahi kufanya hivi, kwanini nisifanye tena?’

Post a Comment

 
Top