0
 Mkuu wa  wilaya  Ruangwa  Jj Mkirikiti  akizungumza   na  mganga  mkuu  wa wilaya Ruangwa
 Mkuu wa  wilaya Joseph Mkirikiti  alisalimia  na  wananchi  wa  kijiji  cha NKOWE wilaya  humo  hivi  karibuni


Fadhula  Milanzi Ruangwa
Mkuu Wa wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi  Joseph Joseph Mkilikiti amepiga Marufuku kwenye shughuli zinazoendana na Vigodolo kucheza staili ya Chura na Funua Dela.
Kauli hiyo ameitoa Leo alipokuwa anaongea na waandishi Habari .Mkuu huyo amesema kuwa katika shughuli za Ndoa,Jando na Unyago kumekuwa kuna mziki maarufu vigodolo ambapo kumekuwa na staili ya kuchezesha makalio maarufu Chura na ile staili ya kufunua Dela ambapo wanawake wakiwemo wasichana wamekuwa wanajifunua Dela na kubakia na nguo za ndani tu.
“Hii no kinyume na maadili ya mtanzania.;kwakuwa inadhalilisha jamii na wao wenyew’alisema  Mkirikiti.
Mkuu  huyo wa wilaya  amemtaka  Afisa Utamaduni Wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa  Hussen Mkambala kufuta vibali vyote vya vigodolo ambavyo vitatumika vibaya kwa kufanya mambo yanayokwenda kinyume na maadili ya Kitanzania.
Mkirikiti ameviagiza vyombo vya usalama kusimamia jambo hili. Esha Chimbanga mkazi Wa Kijiji cha Likangara amekiri kuwapo kwa michezo hiyo ya kucheza uchi au nusu uchi jambo ambayo yeye ameyaona kuwa yanafaa kukemewa pia amesema kama yataachiwa yaendelee yataharibu kizazi cha sasa na kijacho kwani tayari baadhi ya watoto wadogo wanaiga

Mkuu  wa  wilaya  akisalimia  na  Diwani  wa Nnowe  wilayani Ruangwa

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top