0

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXMBGlfLYHQZtgYBWxLimVkCxZ-jwhthvCEmcXfmLl6qbi59icjBjUTEVerbXbI1LugOli4zQYft3-uY_5_5eqzthXsUSEgRWAiffcagd-E8CLk3q4iXR-T254Oszm10JztL7YLLIOLJwl/s1600/IMG_4156.jpg
WAKULIMA wa korosho Wilaya ya Tunduru, wameondokana na umasikini kutokana na kupata soko la uhakika baada ya Kampuni ya Namela General Trade kushinda zabuni ya kununua zao hilo wakulima kwa bei ya Sh 3,757 kwa kilo, ikizishinda kampuni nyingine saba.

Hadi kufikia Novemba 14, kulikuwa na zaidi ya tani 541 zilizoingizwa katika ghala la Chama Kikuu cha Ushirika Wilaya ya Tunduru (Tancu) ambako kampuni hiyo ilipewa kununua korosho tani 400 huku Kampuni ya Machinga iliyoshinda nafasi ya pili katika mnada huo, ikipata kibali cha kununua tani 141 kwa bei ya Sh 3,750.

Post a Comment

 
Top