0
Kiongozi wa Upinzani nchini Gabon Jean PingKiongozi wa Upinzani nchini Gabon Jean Ping
Wapinzani nchini Gabon wamechoma moto jengo la bunge la nchi hiyo baada ya Rais Ali Bongo kutangazwa kuwa mshindi wa Uchaguzi wa Rais Uliofanyika siku ya Jumamosi dhidi ya mpinzani wake mkuu Jean ping.
Kwa upande wake mgombea huyo aliyeshindwa amesema pia vikosi vya usalama vimeshambulia makao yake makuu kwenye mji mkuu Libreville.
Jean Ping aliliambia shirika la habari la ufaransa AFP kuwa vikosi vya ulinzi vimetumia helkopta kushambulia kwa mabomu jengo hilo kabla ya kulivamia.
Amearifu kuwa watu 19 wamejeruhiwa baadhi yao wakipata majeraha mabaya.
Awali, polisi katika mji mkuu wa Gabon, Libreville walitumia mabomu ya kutoa machozi kuweza kuwatawanya wafuasi wa Jean Ping, waliokuwa wamejawa na hasira na ambao wanaamini kuwa matokeo hayo ya uchaguzi yalikuwa ya udanganyifu.
Ni kura chache tu, zilizomuwezesha Bwana Bongo kumshinda mpinzani wake na hatimaye kutangazwa kuwa mshindi, huku eneo analotoka akionekana kupata kura nyingi zaidi.
Ujumbe uliokuwa ukiwakilisha upinzani katika Tume ya Uchaguzi ulitoka nje na kukataa kusaini karatasi, zinazompa ushindi Rais Bongo.
Mwangalizi wa Uchaguzi huo, kutoka Jumuia ya Ulaya, Sara Crozier ameelezea hali ilivyo katika mji mkuu wa nchi hiyo, Libreville, kuwa ni ya wasiwasi.
Familia ya Bongo imekuwa madarakani katika nchi hiyo ya Afrika ya kati kwa takriban miongo mitano

Post a Comment

 
Top