Zari la Ngassa lamuangukia Kiiza
Siku moja baada ya mkataba kati ya Mrisho Ngassa
na Free State Stars ya Afrika Kusini kuvunjwa, klabu hiyo imemsajili
mshambuliaji wa zamani wa Simba na Yanga, Hamis Kiiza.
Msimu uliopita, Kiiza raia wa Uganda aliitumikia Simba na kufunga mabao 24 katika michezo yote msimu uliopita kabla ya klabu hiyo kutangaza kumtema katika usajili wa msimu huu.
Taarifa iliyotolewa na timu ya Free State Stars na kunukuliwa na mtandao wa Kickoff.com, zimethibitisha usajili wa mshambuliji huyo, ambaye pia huchezea timu ya Taifa ya Uganda.
“Kiiza amesaini kuichezea Free State juzi, ni mchezaji ambaye msimu uliopita alicheza Simba,” kilisema chanzo hicho na kubainisha kuwa mchezaji huyo alisaini mkataba wa miaka miwili.
Msimu uliopita, Kiiza raia wa Uganda aliitumikia Simba na kufunga mabao 24 katika michezo yote msimu uliopita kabla ya klabu hiyo kutangaza kumtema katika usajili wa msimu huu.
Taarifa iliyotolewa na timu ya Free State Stars na kunukuliwa na mtandao wa Kickoff.com, zimethibitisha usajili wa mshambuliji huyo, ambaye pia huchezea timu ya Taifa ya Uganda.
“Kiiza amesaini kuichezea Free State juzi, ni mchezaji ambaye msimu uliopita alicheza Simba,” kilisema chanzo hicho na kubainisha kuwa mchezaji huyo alisaini mkataba wa miaka miwili.
Post a Comment