0
SEHEMU YA KUMI NA MBILI
Kweli sikutegemea kabisa macho yangu hayakuweza tena kumuona mjomba, ni muda kidogo tu alikuwa ameshaaga na kuondoka, pasipo hata matarajio yangu.

Taswira ya mama ndio ilinipokea baada ya kumuulizia mjomba, kumbe muda mfupi tu alikuwa ameendoka. Sikutaka sana kujishughulisha na habari zake, wakati huo akili yangu ilishaanza kukumbuka kuhusu kijitabu cha kaka Eddy hivyo nilimuaga mama na kuingia ndani, kutokana na tabia nilikuwa nimejizoesha muda wote wa kukaa ndani mama alishaizoe tabia ile hivyo, hata aikumfanya uwenda kuhisi kitu ambacho muda wote kilikuwa kinanifanya niwe ndani.

Nijitoma ndani, nikiwa na shauku kubwa sana, taratibu niliwasha feni na kulifukuza joto katika namna iliyoleta faraja kwenye mwili wangu huku nikiwasha taa kulifukuza giza ambalo lilianza kutaka kushamili ndani ya chumba changu, kufanya macho yangu kuwa katika ubora wa hali ya juu. Mikono yangu haikuchelewa kupambana kule nilipokuwa nimekiifadhi kijitabu kile. Muda mchache macho yangu yalianza kupambana na maandishi yale, ambayo yalionekana kunipa shauku ya kuliona jambo, muda ambao ulionekana si mrefu.
                                                     ************

Kibao kilikuwa kimeendikwa maneno yalikuwa yamesomeka closed yaani kumefungwa ndio yalipambwa nje ya mlango wa ofisi ile, ambayo sikuwahi kutegemea uwenda kungekuwa kumefungwa kwa muda kama ule, niliangalia saa yangu ilionesha vyema ilikuwa sasa tano kasoro, kwa muda kama ule nilijua wazi uwenda hakuwa mbali muhusika wa ofisi ile ambaye ni mkuu wa chuo kile.
Akili yangu haikuniupa kutoka eneo lile, niliamua kujisogeza kidogo na kuketi kwenye moja ya viti vilivyokuwa nje ya ofisi ile. Ambavyo havikuwa mbali sana na dirisha la ofisi ile. Wakati huo sikujua kukaa kwangu eneo lile kungeleta dhahama kubwa sana kwa upande wangu, dhahama ambayo sikuwahi kuitegemea uwenda ingenitokea katika siku ile ambayo ilikuwa ni moja ya siku muhimu sana katika maisha yangu ya kuipata elimu kwa namna moja ama nyingine.

Niliendelea kusubiri kwa muda kidogo kabla ya ngoma za masikio yangu, kuanza kupitiwa na sauti ambazo hakika hazikuwa mara ya kwanza kuzisikia, ni sauti hizo ambazo zilikuwa zinanifanya ni furahi kuwa na mwanamke aitwaye Irene nikiwa ndani ya jambo ambalo wapenzi wote katika hii dunia, wanalipa kipaumbele na kurifurahia kuliko mambo yote.  Mwanzoni nilihisi uwenda masikio yangu hayakuwa vyema kupokea sauti ile, lakini nilipojisogeza vizuri kwenye dirisha lile sasa sikuwa na haja ya kubishana na sauti zile, ziliendelea kupenya vizuri huku zikiuacha mwili wangu katika namna isiyoelezeka kibaya zaidi ni hata yale maneno ambayo mara nyingi Irene alikuwa akipenda kuyatamka tukiwa kwenye zoezi hilo, niliyasikia vizuri ya kimtoka huku sauti ya kugumia ya kumkuu wa chuo kile ilikuwa ikitoka. Nilijiuliza mara mbili mbili huku nikiwa siamini ya kile nilichokuwa nakisikia.  Maswali mengi yalijengeka kichwani mwangu kabla ya kunitoka neno la kizembe katika hali ambayo hata mwenyewe ilikuwa ngumu kujisikia, ni hilo neno ambalo lilikuwa likiomba eti asiwe Irene wangu, nilijitamani kujicheka lakini kicheko kilikuwa mbali, na hata kingekuwa karibu na mimi hakika kingekuwa kicheko kilichojaa uchungu ndani yake.
Uvumilivu ulinishinda nikiwa pale, niliamua kujitoa mahali pale, kwa miadi ya kurudi kwa muda mwingine, sikutaka kuendelea kusikiliza sauti zile, nilijitoa kinyonge kuliko hata nilivyokuwa nikitegemea. 

Wakati huo kwa mbali kelele za wanafunzi ambao walikuwa uwanjani nilikuwa na pambana nazo, sauti ambazo zilinikumbusha vicheko vya wale wasichana ambao akili yangu sasa ilihusinisha na lile tukio, na kukiri uwenda walikuwa wanajua maana ya vicheko vyao, ambavyo mwanzoni  niliwatoa akili sasa nilijiona uwenda mimi ndio nilikuwa sina akili. Japo niliampa kutojihusicha na msichana huyo lakini, nguvu ya penzi ilikuwa ikininyanyasa.

Kweli ilininyanyasa katika kiwango cha juu sana, miguu yangu ilitetemeka njia mule, nikipambana na ardhi ambayo niliona muda si mrefu ilikuwa inataka kunidhalilisha, katika namna ambayo sikuwahi kuitegemea, na hata nilipojikaza bado nilishindwa. Niliamua kujitoma ndani ya darasa moja ambalo lilionekana liko wazi, taratibu niliamua kuketi kwenye moja ya kiti ambacho kilikuwa kimejitomea kimeza kidogo mbele yake. Ambacho kiliupa hifadhi mwili wangu punde nilipojiweka kwenye kiti, baada ya kukisogeza karibu nami, nilijiinamia chini kwa muda kidogo lakini hatimaye fikra zangu zikasiliti kile kiti huku ikijenga taswira ya mkuu yule wa chuo, na Irene wangu. 

Kabla ya kupingana na kile nilichokuwa na kisikia kwenye dirisha la ofisi ile, ya kuwa hakuwa Irene wangu, roho ya kupingana na lile ilianza kunitawala huku nikitamani kwenda kuhakisha juu ya lile. Ukweli ilinisumbua niliamua kujitoa haraka.

Ajabu sasa, bora ningeiamua kubaki kule kule, nisingehitaji ushahidi wa kile.  Masikio yangu yangetosha kuwa shahidi kabisa.  Maana macho yangu sasa yalikumbana na dhahama ile, ni kweli alikuwa Irene. Macho yangu yaliendelea kupambana na mwanamke yule punde alipokuwa akijitoa kwenye ofisi ile ya mkuu wa chuo, utadhani hakuna kilichokuwa kinaendelea ndani yake. Nikiwa nimesima kwa mbali kidogo lakini umbali ambalo ulikuwa ukiniwezesha vyema kuona vizuri kile kilichokuwa mbele yangu, na uzuri, Irine hakuwa mgeni kwangu.

Nguvu ziliniishi na hata hamu ya kuendelea kubaki ndani ya chuo kile haikuwepo kabisa, miguu yangu ilishaanza kugeuza njia ya kurejea nyumbani huku akili yangu ikiwa nzito kuliko kawaida, mwili ukiendelea kupambana na maumivu ambayo hayakuwa ya mchezo hata kidogo. Mawazo mengi yakiwa yanakikabili kichwa changu nikiwa ndani ya daladala nikirejea nyumbani. Alimanusura nipitilizwe sehemu ya kituo cha nilipokuwa na shuka.

Hali yangu haikuwa sawa hata niliporejea nyumbani, siku nzima kwangu ilikuwa mbaya, ijapokuwa nilijitahidi kuificha sana mbele ya mama ambaye kwa upande wake siku hiyo alionekana kama anajambo ngumu linamkabiri hivyo hakujihusisha sana na mimi na hata mdogo wangu Criss siku hiyo si kumkuta nyumbani, alikuwa amekuja kuchukuliwa  na mjomba, ambaye nilipata taarifa zake punde nilipoona kuna tofauti kidogo ambayo hapo awali haikuwepo pale nilipoamua kumuliza mama ambaye alikuwa akiendelea kujishughulisha japo kiuvivu uvivu, ni kama alikuwa anajua uwenda jambo zito lilikuwa linakwenda kutokea katika familia yetu, ni kweli ni kama alikuwa anajua lakini alikuwa tayari amechelewa. Roho yangu haikuwepo tena dunia, kwa muda ule, maana nilipojitoma ndani, sikuona faida ya kuishi katika dunia. Dunia ambayo katika jicho la kawaida niliona hainitaki kabisa, Kiukweli niliamua kufanya maaumuzi haya, huku nikimsihi Mungu.

Post a Comment

 
Top