0

Mkuu wa mkoa wa Lindi,Godfrey Zambi akizungumza na wanachi wa wilaya ya Liwale

 

Mkuu wa mkoa wa Lindi,Godfrey Zambi amewata wananchi wa wilaya ya Liwale mkoani Lindi kuitunza mikorosho ili kuongeza mavuno na kuuza mazao yao ya korosho kwenye vyama vya misingi vya mazao na amewashauri wakulima kuweza kufungua akaunti kwenye banki ili mazao yao yakiuzwa waweze kupokelea pesa kwa njia banki.

Mkuu wa mkoa huyo aliyasema hayo leo akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhala uliofanyika kwenye viwanja vya Nanjinji katika kata ya Likongowele wilayani hapa.

Godfrey Zambi amewaonya watumisha wa serikali wasijihusishe na ulangazi wa ununuzi wa kangomba na watumishi watakaopatikana na ulangozi huo watapoteza kazi zao na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao, watumishi wanaotaka kujihusisha na ununuzi wa korosho waende kwenye mnada wakanunue.

Bwana zambi aliwaomba wanaliwale kuendeleza kudumisha amani ya Taifa na kuepuka tabia ya kubaguana amewataka wananchi kushirikiana kwa pamoja ili kuweza kujenga taifa pia amekemea wanasiasa wanatoka mkoa ungine kuja kufanya siasa Liwale kitendo hicho hakiwezi kutatua kero za wanananchi hao bali amewataka viongozi wa eneo husika kufanya mikutano kwa  wananchi wao na kuweza kuchukua kero na kuweza kuzitatua.

Wakati wa kampeni wakati wa wanasiasa kunadi sera zao uchaguzi ukishafanyika tunaamisha siasi  zetu bungeni au kwenye mabaraza ya madiwani hatuwezi kulumbana kwenye maeneo ya maendeleo muda wote wale waliochaguliwa waende kwenye mabaraza wakalumbani huko lakini wakazungumze mambo ya maendeleo huko” alisema Zambi

Aliongeza kwa kusema viongozi wa jimbo la Liwale wafanye mikutano kwenye maeneo yao na ndio wanaojua kero za wananchi kuliko viongozi wanaotoka nje ya mkoa husika kuja kufanya siasa kwenye mkoa uingine.

Godfrey Zambi aliwakumbusha wananchi juu ya suala la janga la ugonjwa wa Ukimwi amewataka wananchi kuwa waaminifu kwenye mahusiano yao za ndoa kama watashindwa kuwa waaminifu watumie kinga na amewataka wananchi wasiwanyanyapae  wale wanaoishi na ugonjwa wa Ukimwi.

Katika mkutano huo baadhi ya wananchi waliweza kupata nafasi ya kutoa kero zao kama Rafii Likochelo alisema moja ya kero yake anaidai ofisi ya ardhi fidia ya shamba lake kiasi cha shilingi milioni moja na laki tatu na elfu hamisi (Milioni 4,350,000/=) alidai deni hilo ni la muda mrefu licha ya kwenda mkoani na kupewa barau mpaka sasa hajaweza kupata fidia hiyo. 

Nae Idaya Chikawe alimuomba mkuu wa mkoa kumaliza mgogoro uliopo wa mipaka uliopo katika kijiji cha Kikulyungu katika mgogoro huo umeweza kusababisha madhara mbalimbali ikiwemo kutopotea kwa watu na kusabisha wanawake kupoteza wanaume wao.

Godfrey Zambi aliweza kutoa majibu juu ya kero hizo alisema suala la mgogoro wa mpaka katika kijiji cha Kikulyungu ataushughulikia ndani ya miezi 3 utakuwa umeisha na jana (septemba 5) alielekea kijijini huko na kuzungumza na wananchi na suala la fidia la Likochelo amemuagiza mkuu wa wilaya Sarah Chiwamba kukaa na viongozi wa ardhi na kuweza kutatua kero hilo.

Post a Comment

 
Top