0


Hali halisi ya kupatwa kwa Jua Wanging'ombe Mkoani Njombe

Wananchi wa mikoa ya Njombe na Mbeya hii leo wamejumuika pamoja na wageni waliotoka mataifa mbalimbali yakiwemo ya bara la ulaya kushuhudia tukio la kupatwa kwa jua ambalo katika kijiji cha litundu wilayani Wanging'ombe limeanza kujidhihirisha majira ya saa nne na dakika kumi mpaka saa tano na dakika 58
Baadhi ya waliofika katika kutazama tukio hilo wameonyesha furaha zao kwa kuwa hawakuweza kutazama mwaka 1979 na kwamba wanaamini kuwa awamu ijayo miaka 350 ijayo hawata kuwepo tena duniani  wakati kwa upande wa wanafunzi tukio hili likiwa ni mafunzo kwa vitendo kwa kuwa wamekuwa wakisoma kwa nadharia
Issa Hamadi meneja wa mamlaka ya hali ya hewa Tanzania kanda za nda za juu kusini anasema kwamba tukio la kupatwa kwa jua wameanza kulifuatilia tangu mwezi wa pili mwaka huu mara baada ya kampuni ya masuala ya anga ya nchi marekani kutangaza kuwa kupatwa kwa jua kutaonekana nchini Tanzania
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Dkt. Rehema Nchimbi
Kampuni ya utalii ya UPL SAFARI  kutoka jijini mbeya imefanikiwa kusafirisha watalii 36 kutoka mataifa mbalimbali na meneja wa kampuni hiyo Gabriel shawa akisema kuwa kampuni hiyo itaendelea kulifuatilia tukio hilo kila mwaka ambapo hapo 2017 linataraji kutokea nchini marekani
Serikali mkoani Njombe inataraji kuweka alama ya ujenzi wa mnara na shule ya msingi katika eneo ambalo kupatwa kwa jua kumeonekana kwa asilimia 98 kijijini litundu wilayani wanging'ombe
Katika kipindi chote cha kupatwa kwa jua takribani saa moja hali ya hewa ilibadilika kuwa ya baridi sambamba na uwepo wa mawingu yalisababisha hali ya giza huku watazamaji wakiwa katika makundi kutizama jua kwa kutumia miwani maalumu iliyoletwa kutoka nchini nchini ujermani.
Hali ya kupatwa kwa jua ni tukio la aina yake linatokea pale ambapo miali ya jua hupungua hadi kutoonekana tena na kusababisha sehemu ya uso wa dunia kuwa giza wakati wa mchana. Muda wa kufunikwa kabisa ni dakika chache tu katika eneo husika.

Kupatwa kwa jua kunatokea wakati dunia, mwezi na jua vinapokaa kwenye mstari mmoja mnyoofu wakati mwezi unakuwa kati ya dunia na jua. Hali hiyo inapotokea kunajengeka kivuli cha mwezi kwenye uso wa dunia. Kivuli hicho hufunika sehemu tu ya uso wa dunia. Kutokana na hali hiyo kupatwa kwa jua kwa maeneo yaliyo mengi kunaonekana kwa watu wengi kama kupungua kwa mwanga wa jua.

2.Maelezo ya Kisayansi
Wanasayansi wanaelezea kupatwa kwa jua kama tukio linalotokea na kuonekana katika namna tofauti tofauti mfano; ni kupatwa kwa jua kikamilifu hali ambayo hutokea pale miali ya jua inapotea kabisa katika eneo husika kwa kipindi kifupi. Hali hii inapotokea eneo husika linakosa kabisa mwanga wa jua na kuwa giza.

Aina ya pili ni kupatwa kwa jua kisehemu; hii hutokea wakati eneo kubwa linapopata upungufu wa mwanga wa jua hali ambayo hupungua kadiri mtu anavyokuwa mbali na kitovu cha mstari wa kupatwa kwa jua. Kiwango cha upungufu wa mwanga wa jua hutegemea umbali mtu alipo kutoka kwenye kitovu cha kivuli kamili.

Aina nyingine ni kupatwa kwa jua kipete; hali hii inapotokea mwezi huzuia mwanga wa jua kufika kwenye dunia kwa vile huweka duara la kivuli cha mwezi kwenye dunia na hivyo mwanga wa jua huonekana kama pete. Inatarajiwa kuwa aina hii ya kupatwa kwa jua ndiyo itakayojitokeza tarehe 1 Septemba 2016 katika baadhi ya maeneo ya Bara la Afrika.

Kwa hapa nchini hali hiyo inatarajiwa kujitokeza katika sehemu kubwa ya maeneo ya mikoa ya Nyanda za juu kusini magharibi na maeneo ya kusini mwa nchi. Hata hivyo, watu katika maeneo mengine ya nchi yaliyokaribu na ukanda huo wanatarajiwa kuona kupatwa kwa jua kisehemu yaani upungufu wa mwanga wa jua kwa dakika kadhaa, imetabiriwa takriban kakika tatu (3). Jua linatarajiwa kupatwa wakati wa asubuhi kati ya saa tatu asubuhi na saa sita.

3. Athari zake kwa Hali ya Hewa.
Kwa ujumla hakuna athari zozote kubwa zinazotarajiwa kutokana na hali hiyo. Hata hivyo, upo uwezekano wa kupungua kwa viwango vya joto katika maeneo ambapo kupatwa kwa jua Kipete kutajitokeza. Kwa kuwa tukio hilo la kupatwa kwa jua huchukua muda wa dakika chache tu hali ya joto itapungua kwa haraka katika kipindi kifupi na baadae kuongezeka kurudi katika hali yake ya kawaida. Viwango vya kupungua kwa joto vitatofautiana kulingana na umbali kutoka eneo la kupatwa kwa jua

4. Upekee wa tukio la kupatwa kwa jua
Tukio hili hutokea au kujirudia mara chache sana katika eneo husika. Inakadiriwa kuwa inaweza kuchukua kati ya miaka 350 hadi 400 kwa hali hiyo kujitokeza tena katika eneo litakapotokea mwaka huu 2016. Hii ndio sababu kwa watu wa eneo husika na wanasayansi hili ni tukio la muhimu na kumbukumbu muhimu ya maisha.

Post a Comment

 
Top