0


Mkuu  wa wilaya Lindi Shaibu Ndemanga,ametoa onyo kwa viongozi wa dini na wazazi walio na tabia ya kuoa na kuozesha mabinti walio na umri mdogo,wakiwemo wanafunzi kuacha mara moja mpango huo,vinginevyo Sheria itachukuwa mkondo wake,ikiwemo kuwakamata na kuwafikisha Mahakamani.
  
Ndemanga ametoa onyo hilo jana, wakati anazungumza na watumishi wa Idara mbalimbali wa Serikali na viongozi wa dini,waliopo wilayani humo,katika kikao kazi kilichofanyika kata ya Mtama,na kufanyika ukumbi wa kituo cha maendeleo ya jamii,kijiji cha Mtama.
Ndemanga amelazimika kutoa onyo hilo kutokana na kile kinachoelezwa wapo baadhi ya viongozi wa dini,wakishirikiana na wazazi kufungisha ndoa mabinti walio na umri mdogo wakiwemo wanafunzi wakikatishwa masomo yao,kisha kuozeshwa kwa tama ya kupata fedha za mahali.
Aidha,kiongozi huyo wa wilaya ya Lindi,amesema mzazi au kiongozi yeyote wa dini atakayebainika kufungisha ndoa mwanafunzi anayesoma wa Shule za msingi na Sekondari,watakamatwa na kufikishwa Mahakamani.
Pia,amewaagiza watendaji wa vijiji na kata kwenye maeneo yao, kuhakikisha wanaorodhesha majina ya wazazi na walezi walio na tabia ya kuwakatisha masomo wanafunzi wa kike,na kuwaoza kwa ajili ya tama ya fedha.
 
WANANCI kijiji cha  Kitomanga  wakimsiliza  Mkuu wa wilaya  Lindi Shaibu Ndemanga

Post a Comment

 
Top