Wajumbe wa chama cha Umoja Amcos
Mwenyekiti wa chama
cha ushirika cha Umoja (UMOJA AMCOS) ndugu Hasani Mpako awaonya wakulima na
wanachama hicho wenye tabia ya kuweka
vipande vya matofari, kokoto na mabibo
kwenye magunia wakati wanapozipeleka kwenye maghala wakati wa kuuza.
Onyo hiyo aliitoa jana septemba 24, 2016 kwenye mkutano wa chama hicho kilichofanyika
katika viwanja vya Nanjinji kata ya
Likongowele wilayani Liwale mkoani Lindi.
Ndugu, Mpako alisema moja ya changamoto wanazokutana nazo katika
uongozi wa chama hicho baadhi ya wakulima na wanachama wanatabia ya kuweka vipande vya matofari ,kokoto na mabibo kwenye magunia wakati wanapozipeleka
kwenye maghala wakati wa kuuza hali hii italeta sifa mbaya kwenye soko la mnada
na kuonekana korosho za Liwale hazina ubora kwa uzembe wa watu wachache.
“Kuna watu wengine watumishi wa serikali tumewahi kuwakamata
wameweka vipande vya matofari kwenye magunia ya korosho na wanakuja kuomba
mchana na usiku tusiwapeke kwenye vyombo vya sheria watakosa kazi lakini sasa
watu wenye tabia hii hatuwavumilia ” alisema Mpako.
Katika mkutano huo wanachama wa chama hicho kwa pamoja walikubaliana
na kulidhia na bei ya usafirishaji
kutoka kwenye kituo wanachouzia na kusafirisha mpaka kwenye ghala kuu la mnada
la chama hicho kila kilo moja watakata shilingi 20/= na kuwa na jumla ya ushuri
zote kufikia shilingi 211 na wakulima hao watashirishwa wakati korosho hizo
zitakapouzwa kwa mnada.
Mpako alisema jambo la ucheleweshaji wa usafirishaji kwenda kwenye soko la mnada hatarajii kujitokeza
na mpaka sasa amepokea maombi ya wasafirishaji
ya watu watatu na anatarajia
kuwashawishi na watu wengine ili kuweza kuzifisha korosha kwenye soko kuu la
mnada kwa wakati.
Mwenyekiti huyo akijibu maswali mbalimbali kutoka kwa
wanachama juu ya ucheleweshaji wa soko la mnada alisema swala la kuchewa mnada
ni gumu na halina jibu la moja kwa moja kikubwa kuomba wanunuzi waje kwa wingi Pia
katika mkutano huo Mpako aliwasisitaza wakulima kufungua akaunti banki.
Post a Comment