Zikiwa zimepita siku 67 tangu abebe majukumu ya kuinoa England, Sam
Allardyce kwa ridhaa yake ameamua kujuzulu nafasi yake ya umeneja
kufuatia shutuma nzito za kuonekana kwenye video akitoa ushauri wa jinsi
wa kupindisha sheria za usajili za FA, imethibitishwa.
Baada ya uamuzi huo, bosi wa kikosi cha England cha chini ya miaka 21
Gareth Southgate atashikilia wadhifa huo kwa muda na kuiongoza timu hiyo
kwenye michezo minne ijayo, michezo wa kufuzu fainali za Kombe la Dunia
dhidi ya Malta, Slovenia na Scotland, na ule wa kirafiki dhidi ya
Uhispania.
Mtandao wa The Daily Telegraph lilichapisha kipande cha video
kilichodaiwa kumwonesha Allardyce akiwaambia watu wawili ambao
wanahisiwa kuwa ni kutoka Mashariki ya Mbali kwamba angewapa mbinu ya
kupindisha sheria za usajili wa wachezaji za FA kwa kutumia njia ya
‘third-party ownership’.
Ametuhumiwa kufikia makubaliano ya kulipwa kiasi cha euro 400,000 ili
kuwasaidia katika mchakato huo wa uvunjaji sheria na kuahidi
kuwawaklisha katika baadhi ya matukio ambayo yangehodhiwa na FA.
Allardyce ,61, pia ametuhumiwa kumkosoa mtangulizi wake kwenye kiti cha
umeneja wa England Roy Hodgson na msaidizi wake Gary Neville kufuatia
England kutolewa na Iceland kwenye Michuano ya Euro 2016, huku
akishindilia msumari mwingine kwa kusema kitendo cha FA kutumia gharama
kubwa kuufanyia marekebisho Uwanja wa Wembley ni “upuuzi”.
Allardyce anazidi kuhas England manager’s disease
“FA inathibitisha kwamba Sam Allardyce ameacha nafasi yake kama meneja wa England,” taarifa rasmi ya FA imeeleza.
“Kitendo alichokifanya Allardyce, kama ilivyoripotiwa leo, hakikuwa cha
kiungwana hasa kwa meneja wa England. Amekubali kwamba amefanya kosa
kubwa na tayari ameomba radhi. Hta hivyo kutokana na ukubwa wa shutuma,
kwa pamoja FA na Allardyce wameamua kufikia makubaliano ya kusitisha
mkataba mara moja.
“Huu si umamuzi ambao umechukuliwa kijuu-juu isipokuwa baada ya
kufikiria kwa kina ili kulinda maslahi mapana ya mchezo wa soka na
kuendelea kuufanya mchezo kuendelea kuwa na heshima kubwa.
“Meneja wa timu ya England ya wakubwa lazima adumishe misingi imara ya
nidhamu na kuonesha heshima katika mchezo wa soka kwa nyakati zote.
“Gareth Southgate atachukua nafasi hiyo na kusimamia michezo ijayo dhidi
ya Malta, Slovenia, Scotland na Uhispania wakati huo FA ikianza
mchakato wa kusaka kocha mpya.
“FA inapenda kumtakia Sam kila la heri kwa siku zijazo.”
Post a Comment