0



SEHEMU YA KUMI NA MOJA
Walifanya jambo ambalo sikulitegemea kabisa, kama wangelifaya  kwa upande wangu,  ni vile walivyokuwa wakinitizama kwa dharau kiasi cha kwamba , nilihisi uwenda kuna kitu nimekifanya kibaya dhidi yao, lakini nikakumbuka si kuwa na wafahamu labda wao ndio walikuwa wakinifahamu. Sikutaka kuisumbua akili yangu nilipuuzia, nikiongoza kule kwenye ofisi ya mkuu wa chuo.
Lakini sasa ofisi ilinipokea katika namna ya aina yake, macho yangu yaliweza kuona lile kwa uzuri kabisa, ni kweli niliona.
                                                            ***********
  “Aahhh! nani tena?” , haraka nilijitoa ndani kuelekea nje baada ya kusikia sauti ikiniita jina langu.  Haikuwa ya mwingine, ilikuwa sauti ya mjomba. Nilishangaa ujio wake katika mshangao ambao tayari nilikuwa na majibu nao.
“Karibu anko”, nilimkaribisha kabla ya kumsalimu, wakati huo akikaribia ndani na kuketi katika moja ya sofa. Punde mjomba aliniuliza habari za mama, nikamwambia yakuwa ametoka kidogo, kauelekea kwenye mikutano yao. Hivyo alikubaliana nami na maneno yangu, tuliendelea kukaa pale sebuleni wakati huo, nilikuwa nimempatia maji kama alivyokuwa, ameniagiza.  Aliendelea kunywa taratibu huku kinywa chake kikionekana na mengi ya kusema lakini, katika namna ambayo nilikuwa najua sipaswi kujua kutokana na tabia yake mjomba.
   
Nilikuwa Kimya tu huku sauti ya runinga kidogo ikifukuza kimya kile, kabla yakufukuzwa kwa mazungumzo yetu sasa, tulizungumza sana na mjomba kwa wakati ule, mazungumzo ambayo mjomba aliyatawala sana. Ilikuwa juu ya masuala yangu ya shule, hakuchoka kunisisitiza niendelee kusoma iliniweza kufaulu mtihani wangu, huku akinipa mifano mingi mingi kuhusu maisha. Nami nilikubaliana na maneno yake kwa kiasi kikubwa. Aliendea mbali zaidi na kunikanya kuhusu mahusiano katika namna moja ama nyingine nami nilikubaliana nae kabisa na hata asingeniambia habari za mahusiano kwa upande wangu moyo wangu, haukuwa tayari kabisa kujihusisha ndani ya dhahama hiyo. Ni kweli tangia hapo nyuma sikuwahi kupenda na kuhusu wanawake nilikuwa nikisikia tu kwa watu na kamywe sikuwahi kujua uzuri wa viumbe hivyo zaidi ya mabaya ya viumbe hivyo labda vingenifanya niwe mfuasi kama wa viumbe hivyo kama binadamu wengine. Hivyo pale maneno yake mjomba kuhusu wanawake kwangu niliona hayana tija hata kidogo.
Mazungumzo yetu yalianza kukatishwa na njaa kali iliyoanza kuchachafya tumbo langu, japo nilijitahidi mwanzoni kujizuia lakini hali ilionekana kuleta ugumu upande wangu. Nilijua wazi mama asingeweza kurudi na kufikia kupika, hivyo ilinibidi niandae chakula cha haraka. Akili yangu ikafikiria kwenda kuchukua samaki wa kukaanga ambao hawakuwa wanakaanga mbali na maeno yale ya nyumbani.  Nilivyomaliza kutaarisha ugali. Nilichepuka haraka kwenda kuchukua samaki ambao niliona wangefaa kabisa katika kuridhisha tumbo langu na hata la mjomba. Kuhusu mama sikuwa na shaka nae mara nyingi hakienda kwenye vikao vyao huwa akirudi hanaga mpango wa kula.
Kweli nilifanikiwa kuridhisha tumbo langu baada ya dakika kama kumi, hapo walau maneno ya mjomba yaliweza kupenya vizuri kwenye masikio yangu kwa mara nyingine kuliko hata awali.  Wakati tukiendelea kuzungumza baada ya kumaliza kula, haikupita muda mrefu hatimaye mama alirejea kutoka mkutanoni na kukuta ujio wa mjomba machoni mwake.
Sidhani kama mama alikuwa anategemea mjomba angekuwa pale kwa nyakati ile. Maana ilikuwa ajamaliza hata siku tatu alikuwa amerejea tena. Mjomba alionekana ana mengi yakuongea katika kinywa chake.
Sikutaka kuendelea kukaa pale, baada ya kuzungumza kidogo na mama huku akinipatia maagizo ya kwenda sokoni kwa muda ule, alikuwa kama anajua kuwa nisingeendelea kukaa kusikiliza maongezi yao.
Taratibu niljitoa ndani, miguu yangu ikiongoza soko lilipo, dakika chache tu zilinifanya nifike eneo lile, nilichukua nilichokuwa nimeagizwa na kurejea nyumbani. Wakati huo nilikutana na maongezi yalikuwa yakiendelea kati yake mama na mjomba, sikutaka kuyafatiria. Nilijitoma ndani ya chumba changu baada ya kumkabidhi alichokuwa amenituma.
Nilijibwaga juu ya kitanda nikiwa katika tafakuri kidogo, ni kweli tafakuri ile ilinitoa pale nilipokuwa na kunipeleka mbali zaidi, katika namna ambayo sikudhani kama ingenipeleka mbali. Na kiri wazi ndugu msikilizaji, mawazo ni kitu kibaya sana, hakika ni ubaya ambao uwezi kuoona katika jicho la kawaida.  Mwili wangu ulikuwa pale kwenye kitanda lakini akili haikuwa pale kabisa, hata nusu saa, lisaa linipita nikiwa pale pale juu ya kitanda, huku nikiwa nimeyakodoa macho yangu juu tu.
Naikumbuka siku ile, ndio haikuwa imenipotea, naam!. Mawazo ya shule yalinijia nikiwa kitandani pale.  Haswa nilikumbuka siku ile, nilivyoletewa habari za kupendwa na msichana, haikuwa kazi ndogo katika kutuliza mzuka wangu. Hakuna aliyetegemea uwenda ningezipokea habari zile katika mtazamo wa namna ile, mtazamo ulijaa chuki ndani yake. Na si hivyo tu aina ya msichana mwenyewe ndio ilifanya watu wa nione wa ajabu kweli. Na kiri tena ndugu msikilizaji alikuwa msichana ambaye hakuna mwanafunzi wa kiume wa shule yetu asingependa kuwa nae, Mungu alikuwa amekijalia kiumbe hicho, mwili wa wastani, usiochukizwa kwenye macho ya wapenda ngono.  Lakini kwangu hakupata nafasi walau kumtazama mara mbili mbili na kubadili msimamo wangu.  Ilikuwa bahati nzuri kwake siku hiyo naweza kusema maana lilishia juu juu baada ya fikra zangu, kuamua kulipoteze jambo lile, huku nikitoa onyo kali kwa msichana yule.
Sasa lilikuwa limejirudi jambo lile nikiwa kitandani pale, akili yangu ilikubaliana yakuwa nilikuwa sahihi kabisa katika lile, tofauti hata nilivyokuwa nikidhani. Nilisonya mara mbili kabla ya kuamka na kutikisa kichwa changu, huku nikionya kisinilitee kumbukumbu ambazo hazikuwa na faida kwangu.
Ni muda huo, ambao nilisikia sauti ya mama ikiniita na mimi kujitoa ndani, kiuvivu kwenda kumsikiliza. Hakuwa na jipya sana ilikuwa kama nilivyokuwa nikidhani ya kuwa ilikuwa nyakati ya kutumwa tena. Ndio lazima ingekuwa hivyo maana hapakuwa na mtu wakumsidia kazi pale nyumbani walau dhahama hiyo ya kutumwa tumwa isingekuwa kwangu. Nilijitoa kusikiliza wito, katika nyakati ambazo tayari juu lilikuwa likielekea kuondoka kwenye uso wa dunia. 
Wakati huo macho yangu yalikutana na tabasamu pana la mjomba kuliko kawaida, ni hilo tabasamu ambalo lilikosekana nadhani kwa kipindi kirefu kwake. Macho yangu yalipigwa na kama bumbuwazi, kabla ya kukiri sasa mjomba alikuwa ni yule ambaye niliyokuwa nimezoea, katika siku za nyuma. Moyo wangu ulifarijika sana, nilitamani kuendelea kumwangalia lakini sauti ya mama ilikuwa imeshapita ikiniagiza dukani kuendea chumvi.
                                                           *********
Siku hiyo ilikuwa tofauti sana, nilitegemea ningeweza kurejea mapema nyumbani, kutokea dukani kwa Mangi, lakini nilikuatana na wateja kadhaa ambao walikuwa na mengi mahitaji hivyo ilinisubirisha sana, ubaya akili yangu hakunishungulisha kuliendea duka lingine, na pale nilipokumbuka umbali wa kuendea duka lingine mwili wangu ulinyongonyea na kuendelea kusubiria pale pale. Mvumilivu hula mbivu baada ya dakika kama kumi hivi nilipata nafasi ya kuhudumiwa.
Nilirejea nyumbani, nyumba ilinipokea katika namna ambayo sikuitegemea.

Post a Comment

 
Top