0


Mahakama moja ilimtunuku mwanafunzi Sh600 milioni kwa kumtia mimba mwalimu wake akiwa na miaka 16
–Mwalimu huyo alifungwa kwa mwaka mmoja lakini alikaa jela kwa miezi sita pekee. Binti wao ana miaka mitatu
Mwanafunzi mmoja California, Marekani, atatunzwa Sh600 milioni kwa kuhusika kimapenzi na mwalimu wake na kumtia mimba.
Mwalimu huyo Laura Whitehurst, 31, alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na kijana huyo akiwa na miaka 16 ambapo alipata mimba na kumzalia binti miezi tisa baadaye.
Hukumu hiyo ilitolewa miaka mitatu baada ya Whitehurst kutambulika kuwa alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanafunzi wake.
Mahakama iliambiwa kuwa mwalimu huyo alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanafunzi wengine wawili ambao hawakutambulishwa.
Ilisemekana mwalimu huyo alikuwa akishiriki ngono darasani akiwa na mvulana huyo, na nyumbani kwake kwa mwaka mmoja kabla ya tukio hilo kujulikana.
Mwanafunzi huyo alidai kuwa usimamizi wa shule yake, Redlands Unified School District, ulikuwa ukijua kuhusu uhusiano huo lakini ukakataa kuchukua hatua yoyote.
“Ushahidi unaonyesha kuwa usimamizi ulijua vyema kuhusiana na suala hilo lakini ukakataa kuchukua hatua yoyote,” alisema wakili wa mwanafunzi huyo Vince Finaldi.
Whitehurst alifungwa mwaka mmoja 2013 kuhusiana na kisa hicho lakini alikaa jela kwa miezi sita pekee kwa kuonekana kuwa na tabia njema.

Post a Comment

 
Top